Labels

Monday, June 13, 2016

MAKALA YA WIKI

SAFARI YENU
  Sio hoja wala tija kwa wingi wenu. Yawezasimama kauli au tendo la peke yake likawa na tija mbele ya Mungu muweza. Anzeni sasa, munasubiria nini? Mbona kimya kikubwa. Hamukumzowesha hivyo. Muliyabeba matofali ya nyumba mbovu na kumtupia kichwani bila sababu. Hakustahiki kubaki hai. Shangaeni sasa au hamumuoni?.

Muliwauwa watoto wachanga miaka ilee ya marehemu babu yangu, mukahifadhi NDERE ndani ya mifuko yenu. Wapya waliozaliwa na walezi wao wasiowazaa mukawarambisha NDERE hiyo ya siri, walikuwaje?. Waoneni kwa macho yenu. Mwema akawa mbaya. Mulimuhofia kwa mabadiliko?. Sielewei, ALIZINI?. Jicho la tatu limekufa, musilitegemee.

Muliipanga safari peke yenu, mukamkabidhi yaliyo mioyoni mwenu kwa kumtupia chini. EENHH!!! Shupavu nyinyi!. Mulimgeukia alipokataa kuramba unga wenu. HAMUKUMSACHI?. Alikuwa na ule wa RUTUBA anaubugia peke yake, unaangaza dunia.


Alijinadi na kusema “Haya njooni WATUMWA. Naona yaliyomo ndani ya nafsi zenu bila ya kujielewa. Poleni. Kuleni tena NDERE kidogo. Tafadhali musianguke chini ya miguu yangu. Teteeni huo. Siwalazimishi kuramba wakwangu. Poteeni, WAONEVU wakubwa”. Alighairisha kikao mwalimu Abasi baada ya kuwaeleza hayo. Walijisuta na kuanza kuondoka.                                      ALI S. ALI 

No comments:

Post a Comment