Labels

Monday, June 13, 2016

MAKALA YA WIKI

SAFARI YENU
  Sio hoja wala tija kwa wingi wenu. Yawezasimama kauli au tendo la peke yake likawa na tija mbele ya Mungu muweza. Anzeni sasa, munasubiria nini? Mbona kimya kikubwa. Hamukumzowesha hivyo. Muliyabeba matofali ya nyumba mbovu na kumtupia kichwani bila sababu. Hakustahiki kubaki hai. Shangaeni sasa au hamumuoni?.

Muliwauwa watoto wachanga miaka ilee ya marehemu babu yangu, mukahifadhi NDERE ndani ya mifuko yenu. Wapya waliozaliwa na walezi wao wasiowazaa mukawarambisha NDERE hiyo ya siri, walikuwaje?. Waoneni kwa macho yenu. Mwema akawa mbaya. Mulimuhofia kwa mabadiliko?. Sielewei, ALIZINI?. Jicho la tatu limekufa, musilitegemee.

Muliipanga safari peke yenu, mukamkabidhi yaliyo mioyoni mwenu kwa kumtupia chini. EENHH!!! Shupavu nyinyi!. Mulimgeukia alipokataa kuramba unga wenu. HAMUKUMSACHI?. Alikuwa na ule wa RUTUBA anaubugia peke yake, unaangaza dunia.


Alijinadi na kusema “Haya njooni WATUMWA. Naona yaliyomo ndani ya nafsi zenu bila ya kujielewa. Poleni. Kuleni tena NDERE kidogo. Tafadhali musianguke chini ya miguu yangu. Teteeni huo. Siwalazimishi kuramba wakwangu. Poteeni, WAONEVU wakubwa”. Alighairisha kikao mwalimu Abasi baada ya kuwaeleza hayo. Walijisuta na kuanza kuondoka.                                      ALI S. ALI 

Friday, June 10, 2016

DAHMBI YA MOYO. SEHEMU YA KWANZA-SEHEMU YA TISA

JINA LA KITABU: DHAMBI YA MOYO
MWANDISHI: ALI SULEIMAN ALI(Al-Salmy)
Watsapp: 0777749669
Mawasiliano  :0658745759 



SURA YA KWANZA
Yalikua ni majira ya asubuhi inayojivutavuta kutoka alfajiri, jua lenye rangi nyekundu ndio hiloo linachomoza kutoka mawinguni likiwa linasambaza mwanga mwembaamba katika dunia.
 Ni katika kijiji cha Wasahawa vikionekana vibanda vingi vilivyosheheni pamoja ambapo wamiliki wa vibanda hivyo walikuwa wanavitumia kama ndio sehemu ya makaazi yao. Vilikuwa ni vibanda vilivyo sanifiwa kwa umbo la nyumba vilivyozibwa kwa kutumia udongo mwekundu pamoja na nyasi zilizosimama kutokana na jua la siku nyingi.  
Sauti ya huruma ilisikika kutoka kibandani ikisema
      “Mbaraka!!Mbaraka!!... mwanangu…naomba uamke sasa ili uwahi shambani mapema na pia uwahi kurudi mapema maana leo ni jumamosi ndio siku pekee ambayo unapata muda wa kutusaidia kazi za hapa nyumbani, kwani baba yako ndio kwanza amelala nahisi atakua hayuko vizuri maana sio kawaida yake hii…..”
Ilikua ni sauti ya mama wa Mbaraka akiwa amesimama nje ya mlango wa chumba cha Mbaraka, mkononi akiwa ameshika sufuria lililokua na maji machafu.
              Mbaraka ni kijana mwenye umri usiozidi miaka ishirini na miwili, alikuwa na urefu usiopungua futi 5 na nchi 4, alikuwa ni mweusi wa maji ya kunde mwenye asili ya kibantu. Ni kijana alieumbika kisura na hata kiumbo pia, alijazia nyusi na nywele nyeusi zenye mng’aro kiasi ambacho alikuwa na mvuto wa kila aina kwa waschana wengi.
 Aliitika kauli ya mamaake na kuenuka kutoka katika kitanda cha kamba kisichohimili vishindo vya aina yoyote. Baada ya hapo aliingia chumbani kwa baba yake bila kugonga hodi na kumkuta Mzee akiwa haelewi chochote kinachoendelea katika ulimwengu huu, hii ni kutokana na machofu ya siku ya jana shambani yaliyompatia usingizi mzito. Alimuamsha polepole na kumuaga kwamba anaenda shambani. Mzee Mkata alimuitikia vyema mtoto wake bila kinyongo na ndipo aliendeleza usingizi wake uliokuwa umebakia nae Mbaraka aliianza safari ya kuelekea shambani.
Ardhi ilikuwa kavu sana kutokana na jua kali pamoja na ukosefu wa mvua kwa muda mrefu, hali ambayo ilimsababisha kuchoka mapema na kupoteza maji mengi kwa njia ya jasho.
Ilifika saa tatu, ndipo alikamilisha kazi aliyojipangia kwa siku ile. Hakua na muda wa kupoteza alisogea bondeni zaidi ambako kulikuwa na mto mdogo wenye maji mazuri na baridi yasiyokauka katika chemchem hiyo. Alikoga hapo na kusafisha kila kilchochafuka wakati wa kazi.
Mbaraka Alirudi nyumbani na kumkuta mama yake amekwisha muandalia chai mzuri kutokana na uwezo wao. Ulikua ni muhogo wa kuchemsha na mchuzi wadagaa . Walijumuika pamoja na kujipatia chai iliyoweza kuwasaidia kwa muda wa masaa machache. Hii ni kutokana na umasikini uliokuwa unawaandama kila kukicha.
 Jumapili iliwadia, asubuhi na mapema kama ilivyo kawaida ya kijana Mbaraka huitumia vyema siku hiyo kwa ajili ya kujisomea sana ili kutaka kuukabili vyema mtihani wa kidato cha sita unaomnyemelea kwa siku za mbeleni.
 Alikuwa ni kijana aliyethamini sana maendeleo  yake yashule na kuzidisha juhudi kila siku zilivyoendelea mbele ili kuhakikisha anafaulu vyema na kuendelea na masomo ya chuo kikuu,kwani alikuwa na ndoto za kutaka kuikomboa familia yake  ambayo kwa ujumla imekabiliwa na umasikini mkubwa.
 Kila siku alibuni mbinu mpya ambazo zingeweza kumwongezea hamu na kasi ya kusoma. Kwa kiasi kikubwa alifanikiwa juu ya hilo.
Takriban walimu wote walimpenda na kumthamini sana kutokana na nidhamu pamoja na jitihada zake kwenye masomo, jambo ambalo lingeweza kumletea mabadiliko na maendeleo makubwa siku za mbeleni.
Ilibaki miezi miwili tu Mbaraka kukabiliana na mtihani mkuu wa taifa wa kidato cha 6, hivyo juhudi za kusoma zilikuwa nyingi sana.



SURA YA PILI
   Katika kipindi chote hicho maumivu makali yaliukabili moyo wa Bahati aliekuwa binti mrembo katika kijijicha hicho cha wasahawa, alikuwa ni binti mwenye mvuto wa aina yake ambao uliwafanya wanaume wengi waliokosa heshima na hata wenye heshima kutokushindwa lakusema pindi wanapopishana nae. Alikuwa ni msichana mwenye rangi ya maji yakunde yaliyozidiwa nguvu ya weupe usioisha. Hakuwa msemaji, bali heshima na upole ndio ulitawala katika himaya yake.
 Alikua ni mwenye huruma sana hususani pale anapoona matatizo ya aina yoyote yanamkabili mwenzake, hakujali rangi, kabila wala dini, bali kilichokua mbele yake ni ukarimu.
Alipenda sana kuwa ni binti mwenye elimu ila hakuwa ni mwenye kulifanikisha hilo kutokana na mila na desturi za familia yake ambao waliona ni uovu mkubwa kwa binti wa kike kupewa elimu ya shule, hivyo alikuwa akiishi na wazazi kama mtoto wa nyumbani na kukabiliwa na majukumu pamoja kazi zisizoisha.Huo ulikuwa ni wajibu wake muhimu kutokana na mtazamo potofu wa wazee wake.
Takribani wakaazi wote wa kijiji hapo walimuelewa Bahati kwa sifa zake mzuri alizokuwanazo,tatizo kubwa lililomkabili ilikua ni sifa ya aibu ambayo ilikua  inampa maumivu makali ya moyo juu ya kijana Mbaraka.Aliamini kwamba maisha yake yangekuwa na furaha pale siku atakapokuwa anaishi pamoja na Mbaraka.
Kwa muda mrefu uzuri na mvuto wake ulianza kufifia kama mwangaza wa jua la magharibi kuelekea usiku. Mawazo ya kimapenzi yalimtawala kila wakati katika kichwa chake juu ya kijana Mbaraka ambae hakujua kilichokua kinaendelea katika moyo wa binti Bahati.
 Kila alichokuwa anakifanya katika maisha yake aliona kama hakiendi sawa. Hupoteza muda wake mwingi kukaa chumbani na kumuwaza Mbaraka pasi na mafanikio. Maradhi hayakuwa yakimuacha mkono, kwani mawazo juu ya Mbaraka yalizidi kila kitu juu ya maisha yake.Alikua akipoteza muda mwingi sana kukaa akitafakari ni wapi angeanzia ili Mbaraka aweze kumwelewa na akithamini kile kilichomo ndani ya moyo wake.
 Siku zilizidi kusonga,na Bahati alionekana kuwa tofauti sana mbele ya macho ya mama yake.
 Mama Bahati alianza kujawa hofu juu ya afya ya mototo wake. Baada ya chakula cha mchana ambacho Bahati alishindwa hata kutimiza tonge tano katika idadi yake, ndipo alipoamua kwenda kujitupa kitandani kusudi kumwandama Mbaraka katika mawazo yake.
Mama Bahati kwa siku nyingi hakutaka kulivumilia hilo.Nae aliamua kumfuata chumbani kutaka kujua nini haswa kimemsibu mtoto wake ambae ndio hazina yake ya pekee.
 Alipofika chumbani alimkuta akiwa amejifunika shuka mithili ya mgonjwa alieandamwa na baridi kwa muda mrefu.
 Alimuuliza mwanawe “Bahati mwanangu ulishakufa na kubakia mzoga tu……”
Bahati alishangaa kusikia maneno hayo kutoka kwa mama yake “kwanini mama mbona sijakuelewa?”, Aliuliza Bahati.
 “Kwasababu mwanangu Bahati alikuwa hayupo hivi.Sidhani kama ni wewe,nahisi kuna kitu unanificha kwa muda mrefu sasa au unaujauzito unanitafutia balaa hapa kijijini…?”
 Bahati alijibu kwa upole na heshima kwa mama yake “hapana mama…ila uchovu tu ndio unanisumbua...si unajua ardhi ya shamba imekauka sana, hivyo nakua nachoka sana na si vyenginevyo”.
Mama Bahati  hakutaka kujua mengi kwasababu alimuamini sana mwanawe kwani hakuwa anenda kinyume na maadili yao, hivyo alimpa moyo mwanawe kwa kumwambia  ipo siku yataisha hayo,yote yalikua ni  mapito tu. Aliyaongea hayo na kumuacha mwanawe akiendelea kubaki chumbani na yeye alienda kuendelea na kazi yake ya kusuka na ukili na kumata tumbaku chini ya mti mdogo uliokuwa unaficha mwangaza mkali wa jua nje ya kibanda chao.
 Kiukweli Bahati alikuwa anaumizwa sana na hisia za mapenzi juu ya Mbaraka na tayari yalikuwa maradhi makubwa kwake.
    Mtihani wa kidato cha sita kwa Mbaraka ulikaribia na matumaini ya mafanikio sasa yalianza kupotea.Baada ya taarifa kutoka serekalini kwamba” KWA MUJIBU WA SHERIA ZA KISEREKALI, HATORUHUSIWA MWANAFUNZI YEYOTE KUFANYA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA KAMA HATOLIPAFEDHA TASLIMU SHILING 40,000”
Kiasi hicho cha fedha hakikuwahi kumilikiwa hata siku moja katika familia ya mzee Mkata tangu kuanza kuyafahamu na kuyaelewa maisha yake. Baada ya taarifa hizo kuskika ndipo Mbaraka alianza kupoteza matumaini na ndoto zake alizokuwa amezipanga.
Mawazo ya Bahati yalitawala katika mapenzi ya Mbaraka wakati mawazo ya Mbaraka yalitawala katika kutafuta msaada wa fedha ili kukamilisha ndoto zake.   Kwa vile kijana Mbaraka alikua maarufu sana katika kijijihapo kutokana na heshima zake, basi taarifa za kutokukubalika kufanya mtihani wake wa taifa kutokana na ukosefu wa fedha iliskika kwa kila mmoja kijijini hapo.
“Baba, unadhani ndoto zangu zitaweza kutimia namna hii?, nahisi kuiaga dunia mapema sana babaangu,umaskini wetu ndio sababu yakutaka kusambaratisha matumaini yangu.” Mbaraka alisema hayo kumwambia baba yake wakiwa wameketi nje ya nyumba yao wakitafakari ni wapi wangeapata msaada.
“Usijali mwanangu hakika Mungu anasikia kilio chako wala usikate tama,kwa vile siku bado zipo basi na matumaini bado yapo” alimliwaza mwanawe katika hali hiyo ya msongamano wa mawazo.
Mawazo yaliwatala sana vichwani mwao.Hakuna aliyejua aanzie wapi wala amlizie wapi katika kulikamilisha hilo.
  Mzee Mkata hakukata tamaa katika kukamilisha ndoto za mwanawe kipenzi,Siku ya pili ilipowadia alijaribu kupita kwa majirani ili aweze kuazimwa fedha hizo kusudi alikamilishe hili,kwani alijuwa umuhiu wa elimu kwa mtoto wake,na pia alizijali sana juhudi za mtoto wake.
  “ Ama kweli mtaji wa maskini ni nguvu zake mwenyewe” kauli hiyo ilikua ikimpitia kichwani mwake kila wakati baada yakuona matumaini yanazidi kufifia,hakutaka kukata tamaa,alizidi kujaribu kwa hata asiowajua vyema,lakini kila alivyokuwa akijaribu juhudi hizo hakuweza kupata matumaini kutokana na umasikini ambao ulitawala kijijini hapo.Kwa kiasi kikubwa hakuna aliyeweza kumpatia fedha hizo hata theluthi yake.
Aliamua kurudi nyumbani kwani jua lilikua ni kali sana.
 “mwanangu Mbaraka,sistahiki lawama kwako wala kwa Mungu juu ya hili,nimejitahidi sana,nimedhalilika sana hata kwa nisiowaelewa vyema,lakini nimeambulia patupu”Aliyasema hayo mzee Mkata akiwa amekaa juu ya mkeka pamoja na mke wake,huku Mbaraka akiyasikiliza vyema maneno ya baba yake.
Machozi yaliyokuwa yamejificha kwa kasi yalianza kutiririka machoni mwa mzee Mkata. Mbaraka na mama yake waliwajibika kufuta machozi hayo wakati hakuna aliewajibika kufuta machozi ya Mbaraka na mama yake.
Huzuni ilitawala katika nyumba yao kwani jitihada za wote ziligonga ukuta.
 Kwa vile mapenzi ya kweli hayajifichi hata kwa siri ya moyo wa mmoja wapo,lingeweza kutimia hili baada ya Bahati kusikia taarifa hii.Bahati alimpenda sana Mbaraka kiasi ambacho alikuwa tayari kumpatia fedha hizo kwa siri,hii ni baada yakusikia kutoka kwa watu tofauti kwamba Mbaraka hatoweza kufanya mtihani wake kutokana na ukosefu wa fedha.
   Kwa kipindi kikubwa Bahati alikuwa na fedha hizo ambapo hakuna yoyote aliekuwa anatambua juu ya uwepo wa fedha hizo ambazo aliachiwa marehemu babu yake ambaye alimuusia kuwa asiweze kuthubutu kuzitoa fedha hizo kwa mtu yoyote ila kwa tatizo kubwa ambalo litaweza kujitokeza katika familia tu.Bahati aliyakumbuka sana maneno hayo ya marehemu babu yake yaliyokuwa yakimpitikia kichwani mwake “Bahati mjukuu wangu,nadhani leo ndio hatma yangu,sidhani kama nitaweza kubakia duniani tena,Mola tayari ananihitaji,nimekuita chumbani humu peke yako,naitaji kukuachia kiasi cha fedha na asiweze kutambua mtu yoyote zaidi yako, na pia usijekuthubutu kuzitoa pesa hizi kwa matumizi isp…po..kuwa kw…a tatizo kubwa ambalo litawez..za kuikumba familia yako tu, sawa…kwaheri” kauli hiyo ilikuwa inamjia kila wakati kivhwani mwake.

 Lakini mapenzi yaliuzidi wasia wa marehemu mzee Bakari.Hakua na jinsi ila aliamua kuenuka kitandani na kusogea karibu na kipembe cha chumba chake huku akichungulia dirishani kwamba hakuna aliekuwa karibu na chumba chake ambae angeweza kumuona juu ya kile anachotaka kukifanya.Alichuchumaa chini ya kipembe hicho na kuanza kuchimbua kwa kisu kilichokuwa kirefu sana.Baada ya sekunde chache alifanikiwa kutoa kikopo cha kaure ambacho kisingeweza kuharibiwa na mdudu wa aina yoyote. Alinyanyuka na kusogea kitandani huku akiwa ameshikilia kikopo hicho.Aliketi kitandani na kutoa mfuko ulikuwemo ndani ya kikopo hicho na kuufungua.Alifanikiwa kutoa fedha hizo taslimu ambazo zilikua ni shilingi elfu 40.
  Baada ya hapo aliwaza ni jinsi gani fedha hizo zitaweza kumfikia Mbaraka bila ya Mbaraka mwenyewe kuweza kuelewa kwamba pesa hizo zinatoka kwake.
 “Nifanye nini sasa au nikaziweke chini ya mlango wa nyumba yao?, hapana itakua sio sahihi,naitaji Mzee Mkata tu peke yake ndio aelewe juu ya fedha hizi na si mwenginewe”. Yalikuwa ni maneno yaliyokua yakipita kichwani mwa Bahati.
Ghafla wazo jengine lilimjia kwamaba,kwa vile ilikuwa ni asububuhi ni vyema aweze kwenda shambani kwa Mzee Mkata huenda  akaweza kukutana nae,kwani alielewa kawaida ya mzee Mkata ni  kueda shamba kila siku wakati wa asubuhi.

 Kwa vile alielewa kwamba siku za mitihani zilikuwa zimebaki chache hakuwa na muda wa kupoteza, aliharakia shambani bila ya hata kumuaga mama yake kwamba anaelekea wapi.
 Safari haikuwa fupi na jua lilikuwa kali sana ila hakuweza kuyahisi maumivu hayo ila ni Mbaraka pekee ndiyo alikuwemo mawazoni mwake.

Mawazo yake hayakumpoteza kwani ni kweli Mzee Mkata muda huo alikuwa shambani akiwa analima baada ya kukata tama juu ya pesa ambazo zingeweza kufanikisha ndoto za mwanawe.  Bahati alikaribia shambani na  alisogea juu ya mlima  mdogo akimtazama mzee mkata akichapuka katika kuwajibika na kazi yake ya ukulima wa viazi.Alisimama hapo kwa dakika chache akiwaza atamkabilije mzee yule na pia atamwelewaje kwa atanachotaka kukifanya.

  Machozi yalianza kumtoka Bahati baada ya moyo wake kuzidiwa na mawazo juu ya Mbaraka na shida anazozipata.Kwa haraka alishika kanga aliyokua amejifunga kiunoni, na kuanza kufuta machozi yaliyokuwa yakimtoka kwa kasi.Alisogea kwa mzee mkata na kusimama karibu yake kana kwamba alikua amedhamiria kumuua.
 Mzee Mkata hakushangaa sana hilo, kwani ilikuwa ni kawaida ya mrembo Bahati kupita pale kila asubuhi wakati anapokwenda kondeni kwao.

  “Bahati leo mbona ghafla na kimya kimya, vipi kwema lakini…?” Mzee Mkata alimuuliza.
      “Kwema...Mzee mkata...shikamooo…!!!!”
 “Marhabaa...Mzima?, mbona jana na juzi hukupita kunisalimia..?”
   
      Bahati alianza kupata moyo wakutenda alichokusudia “hapana mzee nilipita wakati kama huu ila sikukuona nadhani labda uliwahi kuondoka..”, alijibu Bahati huku akiwa anatabasamu ndani ya moyo wake.
 Mzee mkata alisema “ni kweli Bahati siku hizo nilikuwa nawahi kuondoka mapema kwasababu nilikabiliwa na kazi kubwa juu ya kijana wangu Mbaraka nilikuwa natafuta wapi ningeweza kupata fedha kwaajili ya malipo katika mtihani wake wa taifa kwani, huna habari …?”
  Bahati akiwa amejiinamia kwa huzuni “ndio niliskia na ndicho kilichonileta hapa, niliskia hilo kwa muda mrefu kwamba hatoweza kufanya mtihani kama hatolipa kiasi cha fedha.Alianza kukitonesha kidonda cha Mkata kilichokuwa kimeshaanza kupona.
  Mzee mkata alianza kujawa na huzuni, kwani alikwishaanza kuyasahau hayo kwa siku chache. Alimtazama Bahati na kuanza kumuona kama adui aliekuja kuisumbua himaya yake aliyoimiliki vyema, hakujua kwamba Bahati alikuja kwa nia njema ambayo ingeweza kumpa furaha daima.
Bila kuchelewa sana Bahati alitia mkono kifuani kwake na kutoa pesa hizo, machozi yalianza kumtoka kwa huzuni kuona kwamba mtu anaempenda sana anateseka katika kutimiza ndoto zake.Hakupenda hata siku moja kuona Mbaraka amefikwa na matatizo.
Alimuangalia utadhani hajawahi kumuona katika maisha yake kwani hakuelewa ni nini kunachoendelea myoni mwa binti Yule.
Wakati machozi yakimtoka bahati, hakusita  kunyoosha mkono wake kwa mzee Mkata, mkono huo ukiwa na fedha taslim sh/-40000 ambazo Mzee mkata alimaliza juhudi zake zote katika kutafuta pesa hizo bila mafanikio.Alikua haamini kinachotendeka,alihisi kama yupo kwenye ndoto.
Wakati Bahati akimpatia Mzee Mkata fedha hizo alimtamkia  “hizi ni pesa taslimu kwaajili ya Mbaraka,naomba umpatie ili aweze kufanikisha malengo yake ya kielimu,ila nakuomba mzeee...naomba siri hii iwe ni yangu mimi nawewe tu,nakuomba...nakuomba...nakuomba kama mzee wangu…fedha hizi zilikua ni hakiba kutoka kwa marehemu babu yangu..”  Bahati alimueleza mzee mkata yote bila kumficha kuhusu wasia wa babu yake juu ya fedha zile.
 Mzee Mkata alisimama kama mnara uliojengwa sikuchache zilizopita. Aliyashayangaa hayo na hakuweza kuongea chochote zaidi kumuahidi Bahati kwamba hatothubutu kumzungumzia yoyote suala hili.Alimshukuru sana na aliona kama ni miujiza kutoka kwa mungu.Hakuweza hakuamini kilichotokea.
 Alimshukuru  sana Bahati pasi na kifani, hakujua atamlipa nini binti huyo wala amshukuru namna gani.Wakati wote huo Bahati hakuweza kuyazuia machozi yaliyokuwa  yakimtoka kwa kasi,na pia hakuweza tena kustahamili kukaa pale, alikimbia na kuelekea nyumbani kwao.
 Haukuchukua muda mrefu, Bahati aliwasili nyumbani kwa kasi ile ile,alipitiliza moja kwa moja hadi chumbani kwake,wakati huo mama yake hakuwepo nyumbani ila alienda kuwasalimu majirani zake kama ilivyo kawaida yake.
 Kwa vile Bahati anaelewa sana wasiwasi wa mama yake pindi amkutapo katika hali hiyo, hakua na budi kujilazimisha kuyazuia machozi yasiendelee kutoka.
 Kadiri siku zilivyokuwa zinaendelea uzuri wa Bahati ulikua unaendelea kupotea na hali yake kiafya ilizidi kuwa mbaya.Kiukweli mapenzi yaliusumbua sana moyo wa Bahati.
“Nitaishi katika hali hii mpaka lini, au kifo changu kinachungwa na mapenzi?, Bahati mimi ,kwanini nisimueleze ukweli Mbaraka, ….atanihukumuje,… hapana, siwezi kumwambia, nitaichukia jamii kwa aibu kubwa” maneno hayo yalikua yanampitikia Bahati ndani ya moyo wake akiwa kitandani kwake.



SURA YA TATU
  Yalikuwa ni majira ya saa tano asubuhi Mbaraka akiwa nyumbani kwao akiendelea kujisomea kama kawaida yake kwa kuamini maneno ya baba na mama yake kwamba asikate tamaa, ipo siku Mungu atasikia kilio chao.
Wakati huo mama yake alikuwa yupo jikoni akiendelea na shughuli zake binafsi.Ghafla alisikia kishindo cha jembe lililoanguka kutoka kutoka katika mabega ya mzee Mkata.Kwa haraka aliacha kazi zake na kuelekea nje ili aweze kujua nini haswa kimemsibu kipenzi cha moyo wake.Alimkuta mzee Mkata amesimama na kuelekea jua na kulipa uso wake huku akiwa ameshika kiuno kwa chake kwa mikono yake yote miwili. Kikweli mpaka sasa alikuwa hajaamini kile ambacho kimetokea lakini uso wake ulionesha kutawaliwa na furaha ambayo kwa muda mrefu ilikuwa imempotea.
Bi Mwenda alimsogelea karibu na kumwangalia usoni hakuna kilichojificha. Aligundua uwepo wa furaha iliyotawala katika uso wa mume wake.
 Bila kumuuliza chochote alichukua jembe na kuliingiza ndani na ghafla alitoka na kumkaribisha mume wake.
 “Haya karibu mume wangu jitayarishe uwahi kunywa chai mana nahisi una hamu na chai ya leo …”
 Mzee Mkata aliitika wito huo wa mke wake na kujitaarisha kwaajili ya chai,baada ya dakika chache alimuulizia Mbaraka kwani alikua na hamu ya kumkabidhi yale yote yaliyo moyoni mwake.
“Mbaraka yupo wapi…? Aliuliza mzee
   “Nadhani atakua ndani kujisomea kwani nilizidi kumuusia kwamba asijaribu kukata tamaa, ipo siku Mungu atasikia kio chake”, alijibu kwa huzuni bi Mwenda.
“Hahaha!!!, Tena nileo” aliongezea mzee Mkata huku akiangua kicheko kilichomshangaza mke wake.
   “Mmmm nawewe nawe, mbona umekuja na furaha leo” aliongea hayo huku akienuka kuenda kumwita mwanawe.
Kwa bahati mzuri Mbaraka hakuwa mbali.Alikuwepo chumbani akiendelea na majukumu ya shule.Bi Mwenda aliwajibika kuwakutanisha wote ili waingize tumboni riziki waliyobarikiwa kutoka kwa Mungu.
Wakati wakiendelea kujipatia chai mzee Mkata alimuuliza Mbaraka,“Ni siku ngapi ambazo zimebakia kuingia katika mtihani?”
 Mbaraka alijibu kwa huzuni bila kujua nini alichokusudia baba yake hata akaamua kumuuliza hilo “zimebaki siku tatu tu baba…”
  Mzee Mkata hakuona haja ya kusubiria, aliwaeleza kwamba tayari amefanikiwa kupata fedha hizo zote na kuahidi kwamba kesho atazifikisha sehemu husika,kwaiyo alimtaka mwanawe aongeze juhudi kwa kujitayarisha vyema kwa mtihani kusudi aweze kukamilisha ndoto zake alizozipanga.
  Bimwenda alijaribu kumuuliza ni nani ambaye amempatia fedha hizo,lakini mzee Mkata hakuonesha kufurahishwa na swali hilo,bali alimjibu mke wake kwamba “daima binaadamu wote hawako sawa,wapo wenye navyo, lakini roho zao ni ngumu kutoa kwa wengine,na wapo wasionavyo lakini mioyo yao ni milaini kutoa,Mungu amesikia kilio chetu”
Bi mwenda hakuridhika vyema na jibu hilo kwani alitaka kumjua mtoaji ila kwavile alimuamini sana mume wake hakutaka kuendelea mbele kwa maswali hayo.
 Kiukweli wote walifurahi kwani walijua mkombozi wao ni elimu ya kijana wao mbaraka juu ya umaskini wao. Hivyo walipaswa kulijali hilo.
Siku iliyofuatia mambo yalienda kama yalivyopangwa, Mzee Mkata alifanikiwa kuzifikisha fedha hizo panapohusika, walimu walifurahi sana waliposkia hilo na pia taarifa haikusita kuenea kijijini kote.
 Siku mbili baadae Mbaraka alikuwa tayari kukabiliana na mtihani huo, kwani alikuwa amejitaarisha vyema kama majeshi yanayoenda vitani kukabiliana na magaidi wa dunia.Furaha ilitawala kila kiungo cha Mbaraka na wazee wake.Wakati huo hali ya Bahati alizidi kudhofu licha ya furaha ndogo kumuingia moyoni mwake kutokana Mbaraka kufanikiwa kulipa fedha zote.
 Masiku yalipita na Mbaraka alifanya mtihani wake ambao ulifanikisha kumuweka katika idadi ya majina ya wanafunzi waliofaulu vyema na kujiunga na chuo kikuu cha Dar es alaam.
 Mzee Mkata pamoja na mke wake bi Mwenda walifurahi sana.Kwa mbali walianza kuiona nchi kavu kutoka katika bahari yenye mkondo mkubwa.
 Muda wote yakiwa yanapita hayo kwa furaha Bahati hakuwa na furaha kwani alijua kifo kinamnyemelea kwasababu afya yake aliyobaki nayo.
Aliamini kwamba uwepo wa uhai wake kwa kipindi chote hicho ilikuwa ni kuwepo kwa Mbaraka kijijini,leo hii Mbaraka anaondoka na hatoweza kumuona tena wala kuskia habari zake kama alivyozoea.Maneno hayo yalikua ndani ya kichwa chake yakimuumiza sana.
Bahati akiwa mwenyewe chumbani alilia sana,ila hakuwa na lakufanya ispokua alienda kumpatia mzee Mkata zawadi ya pete mzuri aliyokuwa nayo mkononi mwake na kumtaka mzee Mkata ampatie Mbaraka pindi aondokapo kuelekea Dar es salaam na amtake ulazima wa kuivaa pete hiyo popote aendapo,hii ingeufanya moyo wake kuwa na matumaini juu ya mapenzi yake.
          “Mzee naomba uchukue pete hii na umkabidhi Mbaraka pindi atakapoondoka kuelekea huko masomoni ila iwe ni siri yetu kama lile la mwanzo, mtake aivae na wala asiivue” alisema Bahati kumwambia mzee baada ya kusalimiana vyema.
Mzee Mkata nafsi yake ilianza kuchunguliwa na wasaiwasi juu ya siri hizi, lakini aliyatazama zaidi mafanikio.
 Aliyafanya hayo kwa siri yeye na mzee Mkata, hilo lilifanikiwa kwa mzee Mkata kumpatia Mbaraka pete hiyo kuku Mbaraka akijua imetoka kwa baba yake. Wakati Bahati akiyafanya yote hayo, Mzee Mkata hakuwa akimhoji sana Bahati kwani alielewa maradhi ya aibu yamemtawala sana binti huyo.



SURA YA NNE
    Mwezi mmoja baadae Mbaraka aliondoka kijijini na kuelekea Dar es alaam ambako ndiko alienda kuendelea na masomo yake ya chuo kikuu.
 Maisha ya mjini alianza kuyazoea na mafanikio katika masomo yake yalizidi kutokana na jitihada zake.
 Walimu wa chuoni hapo takribani wote walielewa juhudi yake na heshima yake pia.Walimpenda na kumjali sana kwa kila hali.
 Alielewa vyema umaskini unaokabili familia yake na kuelewakwamba  yeye  ndio suluhisho la kuikomboa familia yake.Anasa hakuipa nafasi kama ambavyo marafiki zake Josef na Peter walivyokuwa wakimshawishi na kumsifia maisha ya anasa ili ajiingize katika hayo.
Maisha ya chuo hicho yalikuwa yametawaliwa na starehe.Wanafunzi wakike walijiuza kana kwamba wapo kwenye madanguro ya machangudoa wa mitaani.Vitendo viovu kama vile wizi nao pia ulitawala kwa kiasi kikubwa.
 Maingiliano ya kimapenzi na vitendo vya kusagana kwa waschana viliokuwepo.Yote hayo aliyapa kichogo na kuelewa vyema nini ambacho kimemleta chuoni hapo.
       Ilikuwa ni siku ya jumamosi majira ya saa 11 jioni, upepo mzuri uliokua ukitoka mashariki kuelekea magharibi ukipepea na kuisafisha anga ya dunia.
 Mbaraka alikuwa pembeni mwa bustani nzuri ya chuo hicho akiendelea kujisomea kama desturi yake.Baada ya muda kidogo aliskia sauti ya kike itokayo nyuma yake ikisema
 “Mbaraka… Mbaraka…wewe unapenda kusoma!!!”.
Kwa Ghafla Mbaraka aligeuka nyuma ili kuona ni nani aliekua akimuongelesha.Hakuwa mwengine alikuwa ni Rehema mtoto wa tajiri mkubwa sana Dar es salaam.
Ni mwanamke alieumbika kwa sifa zote anazostahiki kuwa nazo mwanamke mrembo.Alikuwa mweupe mwenye rangi yakuvutia na mwenye asili ya kabila la warangi kutoka Kondoa.Kila kiungo chake kilikaa mahala pake na kumpendezesha,umtoe kasoro gani mrembo huyu.Miguu yake minene ya wastani ilimfanya aweze kutembea kwa tambo la kike huku akimega hatua utadhani anaiyonea huruma ardhi ya mwenyezi Mungu.Binti huyu hata umpe nguo ya aina gani ilimpendeza na kumvutia kwa kila aliyemtia machoni.Kwakweli alikua ni chakula cha macho ya wanaume.Wengi walimtongoza na kuambulia patupu.Alikuwa mkarimu na mpole mwenye sauti nyembamba yenye kuleta mwamkokwa rijali wa kiume.
Ghafla baada ya macho yao kukutana Rehema alionesha kutabasamu na kuonesha mwanya wake uliochongeka mithili ya umbo la pembe nne.
 Naye Mbaraka hakusita kutabasamu ili kuonesha kutokuchukizwa na kitendo hicho.Rehema alisogea karibu na kusimama mbele ya Mbaraka mithili ya mlima wa Kilimanjaro.
      “Habari yako Mbaraka Mkata, naona umetulia peke yako unapiga msuli zaidi” Rehema alimsalimia Mbaraka nakumuuliza hayo.
        “Safi tu sijui wewe” Mbaraka alijibu
 “Samahani naweza kujumuika pamoja nawe..?”
Mbaraka alitabasamu kwa mara ya pili na kuonesha vishimo vilivyochimbika katika mashavu yake yaliyoanza kuchipua ndevu kwa mbali kisha alimjibu “bila shaka karibu, unapenda utani Rehema…ulinishtua unajua”.
         Rehema alicheka kidogo na kumuuliza “kwanini ulikuwa mwepesi wa kushtuka kiasi chote hicho, unakua muoga sana”
     “Hahaha...kwasababu ulikuja ghafla, istoshe nyuma ya mgongo siwezi kukuona” alijibu Mbaraka
  “Nisamehe mwaya kwa kukushtua na pia unisamehe kwa kukukatisha shughuli yako ya kujisomea”.Rehema alimwambia Mbaraka.
  Mbaraka hakujali na akamwambia nayeye asijali pia.Rehema alishkuru kwa hilo.
Kimya kikubwa kilitawala kati yao kwa sekunde chache, baada ya muda Rehema alishusha pumzi ndefu zenye nguvu na zilizojaa woga ndani yake.
“Kwanini unapenda kukaa eneo hili kila wikiend, istoshe ukiwa peke yako…?”. Rehema alimuuliza
 Mbaraka alitabasamu kisha akamuuliza
“Ulijuaje wewe ?”
    “Nilijua kwasababu nakua nakuona sana istoshe hata mimi pia nakua napenda kukaa paleee…sio mbali na hapa” huku akimuoteza kwa kutumia kidole chake kilichopambwa kwa rangi ya kucha ya zambarau.
        “Basi inaonesha macho yako yananguvu sana na upeo wake wakuona mbali ni mkubwa” Aliogea Mbaraka.
 Baada ya kuskia hivyo Rehema alitabasamu na kumwambia “sio sana unanionea tu”. Walijikuta wanafurahi wote kwa kicheko.Waliongea mengi na kufurahi.
 Baada ya muda Rehema aliomba kumuuliza swali.Naye Mbaraka hakusita kumkaribisha kwa hilo.“Asante” Alijibu Rehema.
 “Unatokea wapi, namaanisha familia yako iko wapi?”
 Swali hilo kwa kiasi fulani lilikuwa gumu kwa Mbaraka kwani kila akiwaza kuhusu kwao hujawa na huzuni ndani ya moyo wake,hii ni kutokana na hali ngumu ya maisha inayoikabili familia yake,na wala hakupenda hata siku moja atokezee mtu amuulize kuhusu familia yake kwani kila siku zikiendelea kusonga familia yake inazidi kuwa katika hali mbaya ya maisha.
 Ghafla sura ya tabasamu aliyokuwa nalo liliondoka kwa haraka utadhani sio yeye alietoka kufurahi na Rehema muda mchache uliopita. Hali hiyo ilimshangaza sana Rehema na kumfanya ajiulize maswali mengi kwani alijua kwamba yeye ndio atakua sababu ya kupeperusha furaha ya Mbaraka kwa muda mfupi.Aliyahisi mabadiliko ya ghafla yaliyojitokeza hivyo hakusita kumuuliza.“Mbaraka nimekuudhi…mbona umekua tofauti ghafla?”
 “Hapana Rehema daima mitihani ya Mungu haiwezi kumuudhi mwanadamu mwenye kumwamini Mungu mwenyewe” alijibu Mbaraka.
 Rehema alishtuka kuskia maneno hayo “Kwanini unaongea hivyo ” aliuliza Rehema
 Mbaraka alichukua sekunde chache bila ya kuongea chochote kisha akasema “ndio kwasababu hujaniudhi Rehema niko sawa ila ni mitihani ya Mungu isiyoweza kupingika”.Baada ya kuongea hivyo Mbaraka alimuomba Rehema wasitishe mazungumzo kwasababu anataka awahi kipindi cha ziada na muda ulikua tayari umewadia. Rehema kwa kinyongo cha kutoridhika alimkubalia na kumtaka wakutane tena kesho muda kama huu eneo lile lile.Mbaraka hakukataa kwani tabia yake ya kumjali na kumuheshimu kila mtu aliendelea nayo kila alipokwenda.
  “Haraka haraka haina Baraka” hivyo ndio moyo wa Rehema ulivyojisemea kimyakimya.
Usiku wa siku hiyo Mbaraka hakuwa vizuri kimawazo.Akiwa kitandani kwake alikuwa anawaza mengi sana.Alianza kufikiria shida zinazowakabili wazazi wake kijijini.
  Alitambua kwamba yeye ndio tegemeo pekee katika kuleta furaha ya maisha bora nyumbani kwao.Hakua na jinsi zaidi ya kuamua kutoa shilingi laki mbili kutoka katika fedha alizodhaminiwa na serikali ili kesho aweze kuzituma fedha hizo nyumbani kwao. Aliamini kiasi hicho cha fedha kingeweza kuwasaidia kwa kiasi fulani wazazi wake.Fedha ambazo amepata kudhaminiwa na serikali hazikuwa zinakidhi haja ipasavyo ila hakua na jinsi kufanya hivyo.
SURA YA TANO
Juampili asubuhi Mbaraka aliamua kuamka mapema ili ajitaarishe apate kumuwahi mtu ambae atweza kumkabidhi fedha hizo azifikishe nyumbani.
 Kiukweli Mbaraka alikuwa ni mwanaume mrembo sana.Wazungu wanasema handsome boy.Kila siku zilivyokuwa zinazidi kusonga alizidi kuvutia kwa wasichana kwa kila sifa ya uwanaume.Siku ya leo aliamua kutoka kiaina.Alivaa  suruali aina ya jinzi  iliyokuwa na  alama za kuchanika kutoka China,juu alitupia flana nyeusi iliyokuwa nyepesi kiasi cha kuonesha maumbile ya kifua chake kilichojazia. Ilikuwa ni flana yenye mng’aro na yenye picha ya msanii maarufu aliyependwa sana huko Jamaika.Miguuni  alivaa viatu aina raba nyeupe na mistari meusi.Kiukweli alipendeza sana utadhani alikuwa ni mwanamitindo kutoka ulaya.Mkononi alivaa saa aina ya saiko yenye mng’aro wa rangi ya dhahabu na yenye kumeremeta kutokana na rangi yake.Baada ya hapo alijipulizia mafuta yenye kunukia vizuri aina ya ESCADA.
 Alianza kuteremka ngazi kutoka chumbani akiwa anaharakia katika jukumu la kutuma pesa nyumbani kwao,ghafla akiwa anashuka ngazi kutokana na haraka zake alijikuta anagongana na Rehema kwa bahati mbaya.Rehema  aligeuka kwa ghazabu baada ya kupata maumivu makali mgongoni kwake,lakini ghadhabu zake ziligeuka na kuwa furaha baada ya kuona kwamba alikua ni mwanaume anayempenda sana ndie aliemgonga kwa bahati mbaya.
Mbaraka alikuwa mnyonge kwa kitendo kile, alikuwa amesimama kama mgambo aliekuwa katika kazi yake ya lindo la usiku, hakujua aanzie wapi ili aonekane mkweli kwamba hakuwa amekusudia kumgonga.Rehema alikwishajua kwamba hakuwa amekusudia.
Baada ya Rehema kugeuka vyema alishangaa sana kumuona Mbaraka katika muonekano mzuri ambao hajawahi kumuona nao tangia kuanza kumfahamu. Hakuweza kuamini macho yake, alitamani amrukie na amkumbatie kifuani kwake lakini hakuweze kufanya hivyo kutokana na pisha pisha za wanafunzi wengi eneo lile.
“Mbaraka ni wewe lakini?” Rehema alimuliza
  “ni mimi Rehema,samahani sana  sikukusudia kufanya hichi kilichotokea hapa bali yote ni kutokana na haraka zangu na mawazo yasiyoisha kichwani mwangu…”.
 Rehema hakujali kilichotokea nae alimtaka asijali pia.
Alimuuliza“kwanini umekuwa na haraka kiasi hicho unaharakia nini?”
 Kiukweli lilikuwa ni swali lililomchanganya Mbaraka kwasababu lilikuwa rahisi lakini lenye uzito wa kujibu kiupande wake, lakini hakuona kama itakuwa vyema akimficha Rehema ambae alimthaminin kwa kumuuliza hivyo kwa bashasha ya kutaka kujua.
Mbaraka aliishinda nafsi na aliona wacha tu amwambie anaelekea sehemu gani, alimjibu “Naelekea ubungo kwasababu nahitaji kumfikishia mtu huu mfuko nilioushika hapa, nae anaenda nyumbani ili aufikishe kwa wazee” 
Rehema alitabasamu kwani aliona Mbaraka ameanza kumjali sasa.Hakuweza kuelewa ni nini kilichokua ndani ya mfuko ambacho kilikuwa kinaharakishwa namna hiyo. Hakutaka kuliacha nyuma, aliuliza akiwa amesimama kwa kutumia vidole vya miguu yake, wakati huo mikono yake ameiweka juu ya mdomo wake,
  “Tunaweza kwenda wote …,I mean kukusindikiza...?” aliuza Rehema.
Mbaraka  kwa vile alikuwa anachelewa  sana na kuhofia kumkosa mtu ambae aliahidiana nae,hakutaka malumbano na maongezi yaendelee zaidi,aliamua kukubali kuongozana nae.Rehema alifurahi sana.
Wakati wanaharakia kutoka nje ili wawahi, mawazo yao ya kupanda gari yalikuwa yanapingana. Kwani mawazo ya Mbaraka yaliwaza kuwahi gari abiria,wakati Rehema aliwaza ni jinsi gani ataweza kuendesha gari kwa haraka ili kumuwahisha Mbaraka.Kilichomshangaza Mbaraka ni kuona kwamba Rehema alichapuka zaidi yake huku akiwa ameielekea gari aina ya RANGE ROVER yenye rangi nyeusi inayong’aa ambayo ilikuwa imepaki pembeni ya geti la kutokea nje ya chuo.
Mbaraka alishangaa sana na kilichompa mshangao zaidi  ni kuona mkono wa kushoto wa Rehema umeshika na kuning’iniza funguo.Moyo wake ulishtuka na kushangaa kiasi cha kuanza kujiuliza maswali moyoni mwake “hivi ile gari ni ya Rehema au nipo ndotoni”. Moyo wake ulishindwa kujibu swali hilo ispokuwa alipata jawabu baada ya Rehema kufika karibu na kuingia ndani ya gari ile akimsubiria yeye afike ili waondoke.
 Mbaraka  hakuweza  kuamini kilichotokea kwani kwa kipindi chote alichozoeana  na Rehema hakuweza kuelewa kama anaweza kumiliki gari  kama hilo amabalo yeye aliishia kuliona likiendeshwa na watu maarufu sana na wenye utajiri mkubwa. Alihisi kama ndoto za usiku zinamjia wakati tayari alishaamka.
 Kwa haraka Rehema alifungua kioo cha gari na kumuashiria Mbaraka apite mlango wa pili.Mbaraka   alielewa lugha ya ishara iliyotumiwa na Rehema,kwa haraka  alizunguka upande wa pili na kufungua mlango na kuingia ndani.
 Kumbe urembo wa Rehema haukuwa katika muonekano wa mavazi tu bali hata anapokaa popote alipendeza.Ndani ya gari lake mulikuwa musafi na harufu ya aina yake.
Aliwasha gari lake na kutoka nje.Alimuuliza Mbaraka “kwaio ndio tunaeleka ubungo?’
  “Ndio,na muda tulioahidiana na huyo mtu ndio huu unakaribia,nataka nimpatie pesa azifikishe nyumbani” alijibu Mbaraka.
“Nakama hatukumuwahi huyo mtu unaemtegemea basi tatuma kwa kutumia njia nyengine”aliongeza Rehema huku akianza kuingia barabarani.
 Alikuwa akiendesha gari kwa uzoefu na kwa umakini mkubwa,waakati huo Mbaraka alikuwa akimuangalia sana Rehema jinsi alivyokuwa anamiliki gari vizuri akiwa njiani.Alitamani hata siku moja nayeye awe anamiliki gari japo sio kama ya Rehema.
 Kwa dakika chache waliwasili stendi ya mabasi ya mikoa na kufanikiwa kuingia hadi  ndani ya stendi hiyo.Mbaraka alitia mkono mfukoni na kutoa simu aina ya Nokia ya tochi.Alianza kuanza kubofya.Punde tu baada ya kubofya simu hiyo alionekana kijana akichapuka kumfuata Mbaraka pale alipokua amesimama. Rehema alimuona mtu huyo akija kwa kasi lakini hakuweza kujua kwamba ndie ambae ameahidiana na Mbaraka kumkabidhi mzigo.Alifika na kusimama mbele ya Mbaraka
  “Mambo vipi Mbaraka, samahani sana kwa kukusumubua,maana nahisi nimechelewa”,alisema mtu yule aliyekuwa mrefu sana.
  “aahh!!!,hapana ila mimi ndio nimekusumbua sana na nataka nikusumbue zaidi…” Mbaraka alimjibu na kuendelea kumwambia kwamba“mzigo wenyewe ni huu (huku akimuonesha mfuko mweusi aliokuwa ameushika mkononi), nataka unifikishie kwa mzee Mkata”
Yule mtu alianza kunywea kwani gari lilikuwa limeshaondoka na hata yeye alipofika stendi hakuliwahi.Hakuwa na jinsi kumueleza ukweli na kumtaka amsamehe kwa kumsumbua.
Kwa vile urafiki wa kweli haupotei Mbaraka aliahidi kumsamehe na kumtaka asijali kwani alikuwa anajuwa njia gani nyengine ya kutumia ili mzigo ule ufike kwa haraka.Waliagana hapo.
Wakati wote huo Rehema alikua amesimama na kutazama kilichokua kinaendelea.Alijiskia furaha kubwa kuwa na Mbaraka kila wakati.Mawazo yake wakati huo yalimpeleka mbali na kuhisi kwamba tayari wameshakuwa wapenzi.Mbaraka  na Rehema walirudi ndani ya gari yao na  yule mtu kuelekea upande wa pili.
Wakiwa ndani ya gari Rehema alimuangalia Mbaraka usoni na kugundua kuwa hakuna furaha ya aina yoyote ndani ya moyo wake.Kwa vile Rehema alimpenda sana Mbaraka na alipenda kila wakati amuone akiwa na furaha alimtaka waelekee katika kituo cha tigo pesa ili amsaidie fedha hizo kufika nyumbani kwa haraka.
 Mbaraka hakulipinga hilo na alianza kuonesha uso wa tabasamu.Rehema aliwasha gari yake na kuelekea katika kituo cha karibu anachokielewa Walifika Manzese mtaa wa Argentina ndipo walishuka gari na kusogea karibu na kituo cha tigo pesa. Rehema alimtaka Mbaraka afanye mawasiliano na watu wa nyumbani kwao kwa kuwapa taarifa kwamba atatumia njia hiyo na hela zitawafika kwa kupitia mtu ambae Mbaraka alimuelewa. Hakusita kufanya hivyo kwa dakika chache na ndipo alimtaka Rehema afanye mambo yake kwasababu yeye alikuwa haelewi chochote kuhusu utaalamu huo licha yakukaa mjini kwa muda mrefu, kwani hakuwahi kumtumia mtu yoyote pesa kwa njia hiyo.
 Alifungua mfuko aliokuwa ameushika mkononi na kutoa kiasi cha fedha kilichokuwemo ambacho ni shilingi elfu tisiini za kitanzania, alimkabidhi Rehema, bila hofu.
Kwa ghafla Rehema alionekana kushangaa sana baada ya kuhesabu fedha hizo.Mbaraka aliuliza, “mbona hutumi sasa na fedha nimeshakupatia …?” Rehema alishangazwa sana na kiasi hicho kidogo cha fedha ambacho Mbaraka anasumbuka tangia asubuhi kutaka kutuma fedha hizo.Yeye alidhania fedha hizo ni nyingi sana zisizopungua milioni moja, hakuweza kustahamili aliamua kumuuliza kama ambae hakuelewa chochote “ndio hizi, mbona ni chache sana...?”
Mbaraka hakupenda kuulizwa swali hilo kwasababu hakuwa anapenda iwe hivyo,alipenda kutuma fedha nyingi sana ili aweze kuwatunza wazazi wake kwa kiwango kinachokidhi mahitaji yao lakini hakuwa na uwezo huo.Alitamani amiliki mamilioni ya fedha ila zilibaki kama ndoto kichwani mwake,jitihada zake zilifikia  elfu tisiini tu.
    “Usijali Rehema,naomba uzitume hizohizo,then siku nyengine nitakuja kuwatumia tena zaidi”.Mbaraka aliyaongea hayo akiwa katika hali ya huzuni sana,hakupenda mtu yoyote agusie kuhusu familia yake,kwani alikua anaumizwa sana na mateso ya umaskini nyumbani kwao,lakini pia hakuweza kumlaumu Rehema wala kumkasirikia kwasababu aliamini kua Rehema hakua anaelewa chochote kuhusu ugumu wa maisha yake.
Kutokana na hali ile Rehema aligundua ukweli kwamba Mbaraka hakuwa na fedha na ndio mana amelazimika kutuma kiasi hicho cha fedha kwani aliamini kwamba hakuna asiyependa kuifaidisha familia yake, wala hakuna anaependa kuiona familia yake ikiteseka kwa shida za kimaisha.Kwa mbali sasa alianza kuelewa kwamba Mbaraka hakua na hali mzuri kimaisha.
 Baada ya kujibiwa hivyo hakuweza kutuma fedha zile,aligeuka nyuma  na kuingia ndani ya gari,baada  ya sekunde chache  alitoka akiwa ameshikilia kiasi cha fedha zisizopungua laki saba na kumtaka mhudumu atume laki saba badala ya elfu tisiiini.
 Mbaraka alishangazwa na kitendo kile,hakuelewakwanini Rehema anaamua kufanya vile.
      “Kwanini unaamua kufanya hivyo” Mbaraka alimuuliza.
 “Kwanini nawe umeniuliza hivyo au hupendi pesa zangu ziende kwenu...?” nae Rehema alimuliza kabla yakumjibu swali lake.
Mbaraka alimtaka samahani kisha alitia mkono mfukoni na kutoa karatasi iliyoandikwa nambari za simu na kumpa mhudumu.
“Tuma kwenda namba hii”. Alimwambia mhudumu.
 Baada ya dakika mbili mhudumu alimwambia tayari ameshafanya hivyo,na aliwashukuru sana na kuwakaribisha vyema.Rehema hakuwa nyuma nae aliitika vyema na kumshukuru mhudumu kwa sana.Waliingia kwenye gari yao na kuanza kuondoka.Wakiwa njiani Rehema alimtaka Mbaraka afanye mawasiliano na nyumbani ili kuwataarifu kuwa fedha zimeshatumwa. Mbaraka hakusita kufanya hivyo.
Kwawakati ule Mbaraka alikuwa na furaha isiyomfano, kwani alitamani amkumbatie Rehema na kumshukuru kwa alilolifanya.Alihisi kama tu akimwambia ahsante haitoshi na ndipo aliamua kumuuliza “Rehema nikupe shukrani gani mana asante pekee haitoshi”
 Rehema alitabasamu kidogo kisha akasema “hivi mbaraka kwanini unataka unishkuru mimi?, nivyema ukimshukuru Mungu ambae ndie anaestahili kushukuriwa,kwani yeye ndio ameniwezesha mimi kufanya haya”. Mbaraka alihisi kama amechanganyikiwa.
“Shukrani zinastahiki na kwako pia, wakati Mungu nilishamtanguliza mwanzo”alijibu Mbaraka.
Rehema alifurahi sana kuskia maneno hayo kutoka kwa Mbaraka.
 Kwa vile muda ulishaenda sana na majira ya saa saba yalishakaribia Rehema bila kuongea chochote tena kuhusu shukrani alimtaka Mbaraka waende kupata chakula cha mchana katika restaurant moja maarufu sana iliyopo maeneo ya Sinza afrika sana.
 “Daima mtaji wa maskini ni nguvu zake mwenyewe”  Mbaraka alikubali wazo la Rehema bila kipingamizi.
 Walifika eneo hilo na walikula chakula cha mchana.Baada ya kumaliza Mbaraka alimshukuru sana Rehema kwa wema wake ambao amemfanyia tangia asubuhi. Kiukweli Mbaraka alishaanza kuelewa sababu ya yote hayo anayoyafanya Rehema.
“Mapenzi tu ndio yanayomfanya afanye yote hayo” kauli hiyo ilipita kichani mwa Mbaraka mara kwa mara.
 Rehema  alimwambia Mbaraka kwamba  hajiskii kukaa chuo kwa leo  kutokana na machofu pamoja na kichwa kuanza kumsumbua,hivyo alimtaka amrudishe yeye tu halafu mwenyewe atarudi nyumbani.Baada ya kuambiwa maneno hayo Mbaraka hakuonesha uso wa furaha kwani alimzoea kwa muda mchache tu.
 Kwavile hakuwa na uwezo wa kumponesha alimtakia  pole  na alimshauri ameze dawa za maumivu ndipo aende nyumbani.Rehema alifurahi baada ya kuambiwa ameze dawa kwanza, kwani aliona sasa kumbe na mwenzake naye  anamthamini sana na anathamini uwepo wake.
  Rehema alikuwa anajali sana afya yake, alipenda kutembea na dawa kama hakiba katika gari lake la kifahari.Alienda kununua maji katika duka lililokuwepo karibu yao ndipo waliingia ndani ya gari na Rehema kumeza dawa na kuanza kuondoka.
  Wakati walipoanza kukaribia kufika chuo Mbaraka alimwambia Rehema “unajiskiaje sasa?”, huku akimuangalia
         “afadhali,nashkuru sana Mbaraka kwa kuonesha kunithamini…” Rehema alijibu kwa furaha.
  Mbaraka alitabasamu kisha akamuuliza tena “kwani nimekuthamini kitu gani Rehema kinachouzidi wema wako”,
 “Kujali afya yangu inazidi thamani nilokuthamini mimi” Rehema alijibu akiwa na bashasha sana moyoni mwake.Mbaraka alifurahi sana.

 Walifika nje cha chuo Mbaraka alishika mlango wa gari kutaka kutoka,ghafla Rehema alishindwa  kuvumilia,na kuamua kushika bega la Mbaraka.Mbaraka alisita kutoka na kugeuza kichwa chake nyuma kumwangalia Rehema pengine huenda kuna kitu amesahau.Uso wa mrembo Rehema ulikuwa ni wenye huzuni sana,alionesha ishara ya kuwa hawezi kukaa mbali na Mbaraka,alitamani hata amchukue nyumbani kwao ila ni jambo lisilowezekana kwasasa.
 Moyo wake ulishamchagua zamani Mbaraka na anafanya haya yote kwasababu ya mapenzi.Rehema alionesha huruma sana.Aliamua kumuachia Mbaraka na kumsindikiza kwa neno lilompa Mbaraka mawazo muda wote.
 “Karibu Mbaraka. Laiti ungekuwa wewe ungeumia zaidi.”Hayo ni maneno ambayo Rehema alimwambia Mbaraka wakati anataka kutoka ndani ya gari.
 Mbaraka alishindwa kuongea chochote na alibaki kumuangalia Rehema usoni.Nyuso zao wote zilionekana kutoridhika kwa kila mmoja kukaa mbali na mwenzake,ndipo aliamua kufungua mlango wa gari na kumuaga kwa ishara ya mkono uliomaanisha  kwaheri Mungu akupe pole.Rehema alitabasamu na kuamua kuwasha gari na  kuondoka.   
SURA YA SITA
Usiku wa siku ile Mbaraka hakuweza kupata usingizi hata chembe,muda wote aliutumia kuyawaza maneno ya Rehema aliyomwambia wakati alipokuwa anashuka gari.Mawazo yaliuzidi nguvu moyo na ubongo wake.Hakuwa anapenda kumuona mtu aliyemthamini kwa kiasi kikubwa anaumia kwa lolote lile,alijiuliza maswali yaliyomshinda kupata majibu yake.Hakuweza tena kuvumilia,usiku ule aliamua kumuamsha rafiki yake wa karibu aliyekuwa amelala kitanda juu ili aweze kumsaidia katika hili.Baada ya kumuhadisia kila kitu Rashidi alisikitishwa sana na habari hiyo,alihisi kama Mbaraka anamtesa Rehema kwa makusudi kutokana na alivyomueleza kila kitu Rashidi alijua fika kwamba hakuna sababu inayomfanya Rehema ayafanye yote hayo zaidi ya mapenzi.Rashid alikua mtoto wa mjini kama akina Piter na mwenzake, lakini yeye hakua anapenda anasa na ndio maana Mbaraka alimuamini na kumsimulia yote. Alimpa ushauri kwa kumtaka muda huo huo ampigie simu ili kumliwaza kwani ni dhahiri atakua anateseka kwa mapenzi juu yake.Mbaraka alimshukuru sana Rashidi na alimuomba samahani kwa kumsumbua usiku mnene, alimtaka aendelee kupumzika.
Kwa vile Rashid alikua ni rafiki mwema kwa mwenzake nae hakulijali hilo.
   “Bila samahani ila fanya ivyo nilivyokuambia” Rashid alimjibu rafiki yake na akaendelea kulala.
 Mbaraka hakuweza kuamini kwa asilimia zote maneno ya Rashidi kwamba Rehema atakua anampenda, kwani yeye aliamini kwamba atakua anayafanya yote kwa ubinaadamu tu na istoshe alishatambua kwamaba Rehema ni binti wa kitajiri hawezi  kumchagua  maskini kama yeye asie na chochote zaidi ya dhiki na hali ngumu ya maisha.Hapo mawazo yalimzidi sana na alihisi kama Rashidi ndio amabae amezidi kumchanganya.
 Licha ya kutokuamini moja kwa moja maneno ya rafiki yake lakini aliamua kufanya kama alivyoshauriwa kwamba ampigie simu Rehema kwani atakuwa anateseka sana kwaa ajili yake.
  Kumbe maneno ya Rashidi hayakuwa yameenda upande kwani wakati wote huo naye Rehema hakuwa katika usingizi zaidi ya kumuawaza Mbaraka kwa kila hali.Alikua anaumia sana ila hakua na lakufanya zaidi ya kuwaza kwamba pindi atapoamua kumwambia ukweli asingemfikiria kwamba yeye ni Malaya.
ALIJIULIZA sana hilo. Hakujua Wapi aanzie na pia aligundua kwamba iwapo atajinyamazia kimya na kuyalimbikiza moyoni basi yangemuumiza moyo wake na pia ataweza kuandamwa na ugonjwa wa mapenzi utaosababisha hata kupoteza dira katika masomo yake. Aliwaza na kuwazua,ila alikumbuka kwamba haraka haraka haina haraka hivyo alihisi ni bora asiliharakie hili.
Kila alipojaribu kulitoa akilini ilimuwia ugumu sana kwani moyo wake ulishapenda. Ghafla alikumbuka msemo usemao kwamba “ngoja ngoja yaumiza matumbo”. Aliamua kukamata simu yake aliyokuwa ameiweka chini ya mto wa kulalia na kuanza kuipiga simu ya Mbaraka.Wakati alivyokua akijaribu kuipiga ilikuwa inakata njiani kana kwamba ilikuwa busy.Tukio hilo lilizidi kumuumiza moyo wake  kwani alihisi kwamba kukatika kwa simu hiyo hakukua na sababu nyengine zaidi ya  Mbaraka alikuwa bize na wanawake wengine.
Usilolijua ni sawa na usiku wa kiza kwani wakati huo nae Mbaraka alikuwa anapiga simu ya Rehema nayo ilikuwa inakata njiani.
 Mbaraka aliamua kuwacha simu ili apumzike kama angeweza kupata usingizi. Rehema hakuchoka kujaribu kuipiga tena simu ya Mbaraka na ndipo kwa mara ya mwisho simu iliita. Mbaraka alifurahi moyoni baada ya kuona kuwa ni Rehema ndie aliekuwa akipiga simu usiku ule. Aliipokea lakini kabla ya yote alitaka kujua anaendeleaje na kichwa kilichokuwa kikimsumbua mchana.Rehema alifurahi kuulizwa hivyo “asante my, naendelea vizuri punde tu baada ya kusikia sauti yako” Rehema alijibu akiwa na faraja moyoni mwake.
Mbaraka alitabasamu baada ya kusikia hivyo, kisha akamwambia “ha ha ha…alafu wewe unapenda uchokozi sana,hivi kwanini sauti yangu iwe ndio dawa yako?”
  Rehema hakutaka kuficha chochote na aliona huo ndio muda pekee wakulifikisha lile lililomo moyoni mwake kuliko kufuga maumivu ambayo yataweza kumuumiza kila wakati.
 “ Kwasababu moyo wangu umekuhifadhi wewe na  wewe na ndio mana ninapoumwa jua furaha yangu imepotea moyoni,ila sauti yako ndio imerudisha furaha hiyo kwasababu ni wewe pekee ambae upo moyoni mwangu” Rehema alijibu bila aibu,kwani hakutaka tena kuficha maradhi yake mbele ya daktari bingwa.
 Sasa Mbaraka alianza kuyaamini yale maneno aliyotoka kuambiwa na rafiki yake.Mbaraka alifurahi sana.
“ kwanini mpaka muda huu hujala?” Aliuliza Mbaraka
kwasababu kuwepo mbali kwako ndiyo sababu inayonifanya nikose usingizi,na ndio maana nimekupigia wewe ili unipenusingizi wangu” alijibu Rehema.
Kwavile alikua ni binti wa mjini hakushindwa na lakusema kwani mjini daima kuna mengi.
   Mbaraka alianza kushangaa na kuhisi kwamba maneno yale  hayakuwa yanatoka moyoni mwa Mehema labda alikuwa na kitabu kilichoandikwa hayo pembeni. “asante Rehema,nimefrahi kuskia hivyo lakini naomba nikulize kitu”
   “Bila shaka, uliza tu” alijibu Rehema.
     “Kwanini uliamua kunizuia pale nilijaribu kuteremka gari na kuonesha kutoridhika na kitu Fulani?”.
 Swali hilo lilikuwa zito sana kwa Rehema kwani jawabu lake ndio lilikuwa kiini cha thamani yote aliyokuwa akimuonesha,aliamua kukaa kimya kwa sekunde chache.  Mbaraka alihisi anaongea peke yake,aliamua kumwita ili aamini uwepo wake kwa wakati ule.Rehema  aliitika na kumwambia  “naomba unisamehe Mbaraka kwani jawabu la swali lako hili litaweza kukuudhi na inawezekana hutotaka tena kuniona katika upeo wa macho yako,naomba  usije  ukanifkiria tofauti kwa kuongea ukweli uliomo ndani ya moyo wangu...”
 alivuta pumzi kidogo kisha akaendelea,“ukweli nikwamba  nakupenda sana na nahitaji uwe dira njema  katika maisha yangu,nilianza kuteseka juu yako kwa kipindi kirefu sana na nilistahamili maumivu ila sasa nimeshindwa na ndio maana nilikwambia naumia sana na maumivu yangu yataondoka pale tu utakapotamka kutoka moyoni mwako kama unanipenda,nisamehe Mbaraka kwani nilihisi kama ulikua unanionea na kuzidi kuniumiza kwasababu nilikuonesha ishara nyingi kwamba tayari ulishakuwa  umehifadhiwa moyoni mwangu...” Rehema alianza kujawa na huzuni kila alipozidi kuongea.
   Nae Mbaraka alianza kutowa na machozi na kuhisi kwamba kumbe angeweza kumpoteza mtu muhimu sana katika maisha yake,hakuwa aliyeelewa chochote kuhusu ishara hizo na alimtaka Rehema asiongee mengi  kwani machozi yalikua yameshafika mashavuni mwake na angezidi kumzidishia huzuni.Alimwambia  “naomba unisamehe sana Rehema,katika kipindi chote  hicho mimi sikuweza kuelewa chochote kuhusu moyo wako,na kwanini usingechukuwa uamuzi huo zamani tu wakuniambia?,am sorry Rehema  naomba tuongee  kesho sasa hivi  muda umeenda sana,na  istoshe mimi nalala na wenzangu humu,hivyo haitapendeza  wakiyaskia haya”. Rehema  alihisi anaonewa kwa  kucheleweshwa kujua ukweli ila alimuelewa Mbaraka na kumwambia “bila shaka,ila kesho wazazi wangu watakuwa na ziara nje ya nchi kwahivyo nakuomba tuwe pamoja nyumbani nadhani  tutaweza kuongea vizuri.Naomba unithamini Mbaraka kama ninavyokuthamini na unijali pia,nadhani inaweza kupunguza maumivu ya moyo wangu”.
Mbaraka hakupendelea sana kuenda sehemu asipojulikana,ila angefanyaje na hataki kumuumiza mtu aliyejitolea kumthamini.
Alimuahidi kuwa watakuwa pamoja.Rehema alitabasamu na kukata simuhuku akitamani kukuche ili aweze kuwa pamoja na ampendae.
SURA YA SABA
  Asubuhi ilipofika Rehema akiwa ndani  ya jumba lao la kifahari,alikua wakwanza kuamka na kufanya usafi kama ilivyo desturi yake awapo nyumbani.Baada ya muda mfupi na wazazi wake pia waliamka kwa lengo la kujiandaa na safari kwani haikuwa ni safari ya karibu. Hata ilipotimu saa mbili kamili Rehema alikuwa tayari ameshawaandalia wazazi wake chai na kuwahimiza kuwahi mapema. Aliwaharakisha makusudi ili awe mkweli juu ya ahadi aliyoahidiana na Mbaraka.  Wazazi wake hawakuwa wavivu juu ya hilo, wote walijitahidi kuwahi mezani wakiwa wameshajiandaa kwa kila kitu.
 Bila ya kupoteza muda walipata chai iliyokuwa imeandaliwa vyema na mtoto wao.Walimaliza na kumtaka Rehema awasindikize ili kusudi aweze kurudi na gari nyumbani.
  Majira ya saa tatu na robo Rehema aliingia chumbani na kubeba begi lililokuwa limeandaliwa vyema na kusheni nguo ambazo zitaenda kutumika waendako. Wote waliingia ndani ya gari na walimuamuru Janeth ambae alikuwa ni mfanyakazi wa ndani afungue geti pindi watakapotoka.
 Safari ya kutoka hapo na kuelekea uwanja wa ndege wa taifa ilianza.Hazikupita dakika nyingi Rehema aliwasili uwanjani na kuagana na wazazi wake kwa huzuni kwani alikuwa anawapenda sana  kama walivyokuwa wanampenda mtoto wao wa pekee. Lakini hakuhuzunika sana kwasababu haikuwa safari ya milele bali ilikuwa ni yamuda mchache tu.
 Baada ya kuhakikisha ndege imeshaondoka hakuwa na sababu ya kukaa sana hapo kwani alihitaji kuzidisha uaminifu wake kwa Mbaraka, aligeuza gari na kuanza safari ya kurudi nyumbani kuonana na yule anaeutawala moyo wake kwa sasa.  Wakati huo naye Mbaraka alikuwa anajiandaa ili kutimiza ahadi alioisaini usiku wa jana.Alienda kukoga na kuanza kujitayarisha kwa mavazi mazuri na manukato ya Dubai.
  Kwa vile Rehema hakuwa anaishi mbali na chuo basi nae Mbaraka hakuwa na wasiwasi moyoni mwake kwamba angeweza kuchelewa.Alianza kujitoa kimtoko. Kilichobaki ni kumuaga rafiki yake kwamba anaenda kuonana na Rehema nyumbani kwao. Rashidi alimruhusu na kumuachia ziada ya maneno kwamba  asije kumuudhi Rehema kwani anampenda sana na ni Bahati kupendwa na mrembo kama huyo mwenye utajiri mkubwa nyumbani kwao.Mbaraka alikirii kutofanya hivyo kwani tayari nae ameshaanza kumpenda Rehema.Aliteremka ngazi na kuelekea nje.Alifika nje ya chuo na kuchukua bodaboda ili jasho lisijekumuharibia manukato yake.
Rehema nae punde aliwasili nyumbani huku akitarajia kwamba atakuwa amemuudhi Mbaraka kutokana na foleni za barabarani zilizomfanya kuchelewa kidogo lakini haikuwa hivyo kwani Mbaraka alikuwa hajafika kwa wakati huo.
 Aliingia chumbani kwake akiwa hana furaha kwani alijua kwamba maneno ya Mbaraka hayakuwa na ukweli ndani yake.Hakua amefika mpaka sasa.Aliamua alijitupa kitandani kwa hasira baada ya kuangalia saa yake ya mkononi iliyomwambia kwamba ni saa nne na dakika 35.
Machozi yalianza kumtoka.Alijua kwamba Mbaraka hajaweka matumaini ya upendo juu yake, alihisi uchungu wa moyo na asijue lakufanya.Alishika simu yake ili amtumie ujumbe mfupi kwa msukumo wa hasira zake na uchungu wake aliokua nao wakati ule.Ghafla aliskia honi ya pikipiki nje ya nyumba yao,alinyanyuka kutoka kitandani kwa haraka na kusogea dirishani ili aweze kuona kwamba alikwa yeye au lah.Kutokana na ukubwa wa nyumba yao hakuweza kuona chochote kilichokuwa nje ya geti.
Aliamua kutoka chumbani kwa haraka na kukimbilia getini aende kufungua kwani  huenda alikuwa ni Mbaraka.
  Moyo wake haukumdanganya kwani alifika na kufungua geti ndipo alipomuona ampendae kwa dhati akiwa anajipangusa mavumbi kwenye viatu vyake.Ghafla nae Mbaraka alitupa macho yake mlangoni ili kuona nani alikuwa muhusika wa kufungua mlango huo,haikuwa mategemeo yake kumuona Rehema akiwa ameshikilia geti huku akimuashiria  kwa macho kwamba kulikuwa na sababu iliyomfanya  amwage  machozi,hii ni baada ya kuona ishara ya macho yake  kuwa mekundu. Alikuwa na furaha baada ya kumuona Mbaraka, “karibu nyumbani Mbaraka,nahisi umechoka sana mana umetapakaa mavumbi sana”,Rehema alisema.
  “Asante”,Mbaraka alimjibu na kumtaka samahani kwa kuchelewa hadi kuyafanya kumfanya macho yako yafunguke kwa wingi kwa kilio.
 Rehema alimuangalia Mbaraka kwa macho ya mahaba na kumtaka asijali kwa hilo.Mbaraka hakuwa ametuliza kichwa chake tangu aingie ndani  ya jumba hilo,alihisi kama ameingia ikulu,hakuwa na mfano wa kuifananisha nyumba hiyo kwauzuri na ukubwa wake.
“Karibu na ujiskie upo nyumani” Rehema alimkaribisha huku akionekana akiwa na furaha sana.
Mbaraka aliketi juu ya sofa la aina yake ambapo tangia kuzaliwa kwake hii ilikuwa ndio mara yake ya kwanza kuona sofa kama hilo.Alianza kuangaza macho macho yake kama ambae hakuwa anajielewa yupo sehemu gani.Rehema aliligundua hilo kwa mbaraka na kumtaka apunguze wahaka hayo ni mambo tu ya kawaida.
 Mbaraka alitabasamu na kupumua kidogo huku akimuangalia Rehema kwa kutokuamini kwamba ipo siku ingeweza kutokea Rehema kumkaribisha kwao kwa heshima zote.
Wakati huo Rehema alikuwa ameshughulika kuandaa chai mzuri kwa ajili ya mgeni wake.Ilikuwa ni chai ya aina yake ambayo haijawahi kuingia katika kinywa cha Mbaraka tangia kuzaliwa kwake.Aibu haikumuacha mkono.Dakika chache zilipita na Rehema alisogea mbele ya Mbaraka na kumsimamia kama anamdai deni la muda mrefu ambalo alimgomea kumlipa.
 Alimtaka asogee mezani ili akajipatie chai iliyoandaliwa kwa ajili yake.Mbaraka alisogea mezani.
Ilikuwa ni meza kubwa yenye umbo la mviringo iliyotengezwa kwa kutumia kioo kitupu ambapo ulieweza kuona kila kitu kilichokuwa chini ya meza hiyo.Aliketi juu ya kiti akiwa na woga kwamba kiti hicho kisingeweza kuhimili uzito wake kutokana na wembamba wa kiti hicho cha kioo.Ushamba ulimuandama kwa kiasi kikubwa.
  Wakati wote huo Rehema alishakaa juu ya kiti akiwa anamuangalia Mbaraka kutokana na uzuri aliokuwa nao,hakuwa anaridhika  kila alipokuwa akimtazama. kwa muda mawazo yake yakampeleka mbali na kuhisi kama yupo kitandani  na mwanaume huyo. Ghafla aliskia sauti ikisema “mbona unachelewa?”, haikuwa sauti ya mtu mwengine ila ni Mbaraka baada ya kuona Rehema yuko mbali kifikra. Aligutuka ghafla na kumwambia“samahani Mbaraka… niliwaza kitu cha kifamilia hapa mana…nimeanza kumkumbuka sana mama yangu”.
   “Pole watarudi tu” alijibu Mbaraka.
  “Asante...karibu chai Mbaraka jiskie upo nyumbani wala usione aibu”.
Walianza kunywa chai huku kila mmoja akimwangalia mwenzake usoni kama kwamba hawajawahi kuonana hata siku moja katika maisha yao. Mtazamo wa mrembo Rehema ulilenga moja kwa moja juu ya kilele cha mahaba na alianza kulegeza macho yake.Wakati  huo mtazamo wa Mbaraka kwa Rehema ulikuwa ni wa kutoamini kama ipo siku angeweza kupendwa na mwanamke mrembo kama huyo  mwenye kila kitu na asiekuwa na shida zaidi ya kuzidiwa na raha za kila aina.
 “Hongera Rehema kwa chai tamu...kumbe umesomea mapishi eenhh!!,tena nadhani sio ndani  ya nchi hii…”,Mbaraka alisifu.
  “mmhh!!! Unaanza sasa matani yako”, Rehema alitabasamu na kufurahi kuskia maneno hayo matamu kutoka kwa Mbaraka.
 “Napenda sana kupika…na hata nikiwa off days huwa namsaidia dada wa kazi katika suala la kupika na ndio mana umeridhika na chakula change, asante”.
SURA YA SABA
  Mbaraka alianza kujiskia uhuru sasa, alikunywa chai na kumwambia Rehema tumbo lake limeshajaa chai tamu,akimaanisha ameshashiba.Rehema hakupinga kwani hata kabla ya kuongea hivyo alishamuhisi kwamba tayari ameshashiba. Alimruhusu anawe mikono.Walimaliza kunywa chai na kupiga story zao za kimasomo.
Bila ya aibu ghafla Rehema alimtaka Mbaraka waingie chumbani ili wakaongelee mambo yao humo kwa kumuhofia Janeth kujua kinachoendelea kati yao.
 Mbaraka alianza kujawa hofu ila alikumbuka maneno ya swahiba wake kwamba asisubutu kumuudhi Rehema kwani hiyo ni bahati ya pekee.Alikubali na wakaingia chumbani.Mulikuwa na kitanda cha aina yake,alifikiria aweze kufananisha na nini thamani ya chumba kile,aligundua thamani yake ni sawa na ikulu ya viongozi wa nchi zilizoendelea.Rehema alimuangalia Mbaraka na kugundua  anahisi  joto kiasi,alivuta pumzi ili kuondoa woga na kumwambia aingie  chooni aende kupunguza joto kwa kujimwadia maji.Mbaraka  alikaa kama  alikuwa anasubiria kauli hiyo itoke  kwani joto lilikuwa linamsumbua sana licha upepo wa kiyoyozi kilichotumika chumbani humo.
Aliingia chooni kama alivyokuja wala hakuvua chochote.Rehema alitaka kuitumia nafasi hiyo ili aweze kuona maungo na mwili wote wa mwanaume huyo.Hisia za mapenzi zilimzidi Rehema baada ya kuskia maji yakiwa yanamwagika chooni, alitumia akili yake kujenga picha kwa kile kinachotendeka humo.Wakati wote huo alikuwa na bashasha nafsini mwake ya kutaka kujua jawabu lake kutoka kwa ampendae.
Baada ya akika kadhaa Mbaraka alitoka.Rehema alinyanyuka na kumsimamia mbele yake mithili ya watu wanaotaka kupimana nguvu,ghafla bila kuhofia alisema  “tafadhali Mbaraka unakumbuka ahadi yetu ya usiku wa jana naomba unijibu ili niupe faraja moyo wangu…”,
 Mbaraka aliuangalia uso wa Rehema kwa matao ya chini kama aligundua amekosea kitu kisha alishika mikono yake na kumuuliza “hivi Rehema  kwanini  unakuwa mgumu wa kuelewa na kumtambua mtu…?,nisingefanya yote haya kama siko tayari kuwa nawewe  kwani ulishanieleza muda mrefu kama unanipenda…”.
 Rehema hakuamini kama Mbaraka angesubutu kumshika mikono yake na kumwambia maneno mazuri kama yale.Alitabasamu kisha akamuuliza “unamaanisha nini?”.
Mbaraka alijibu “namaanisha hatua yangu inakanyaga kila ukanyagapo mguu wako, nimekuja hapa si kwa lengo jengine lolote ispokuwa nadhani Mungu ameshatuandika  tufe pamoja…nakupenda sana Rehema”.
  Rehema hakuweza kuamini anachokisikia,alihisi kama kuna malaika aliyetumwa na Mungu aje amchukue na kumpeleka peponi.Ghafla aliamua kumsogelea zaidi na kumkumbatia.Machozi yalimtoka kwa furaha na ule uchungu wa kuteseka kwa muda mrefu ulipotea ghafla.Mbaraka alimtaka Rehema asiruhusu chozi lake kudondoka kwani linamuumiza sana.
 Kiukweli Rehema anampenda sana Mbaraka.Na sasa Mbaraka ameshaukabidhisha moyo wake kwa mwenzake.Walikumbatiana kwa muda huku kila mmoja akiwa na furaha ya kumpata yule ampendae.
Baada ya dakika chache Rehema aliunyanyua uso wake kifuani kwa Mbaraka na kumuangalia usoni ndipo alipoona machozi yakitiririka kutoka machoni mwa Mbaraka.Alienua mkono wake na kuyapangusa.Furaha yao ilizidi kifani na kujikuta kila mmoja anaangua kilio cha upendo wenye furaha.
Rehema alimwambia Mbaraka “naomba nitimize ahadi nilioweka kwa Mungu”
Mbaraka alishangaa na kujiuliza maswali bila kupata jawabu,“ahadi gani tena mpenzi wangu” Mbaraka aliuliza kwa hisia.
 “Niliweka ahadi kwa mungu kwamba endapo siku utakubali ombi langu basi nakukabidhi nyumba yako binafsi, kwasababu tayari nilishakuamini kwa kila kitu”.Mbaraka alifungua macho yake yote na kushangaa,alihisi kama anaota akiwa amesimama mchana ule,“nyumba!!!” Aliuliza kwa msangao.
 Rehema alijibu “sio nyumba tu na hata uhai wangu”.
Kwa asilimia mia moja Mbaraka alizidi kuyasadiki maneno ya rafiki yake.Alimkumbatia Rehema na kumwambia kwa sauti nyepesi pembezoni mwa sikio lake la kulia“Rehema daima nautambua upendo wa dhati unapopatikana.Nimegundua upo kwako na ninakuahidi kukutunza daima wala sitakuacha labda Mungu pekee achukue uhai wangu mapema kabla yako”.
 Rehema alizidi kufurahi na kuzidi kuung’ang’ania mwili wa mpenzi kana kwamba hakutaka abanduke kifuani kwake.Walianza kujikuta wanaanza kufanya vitu tofauti.Kila mmoja alianza kutembeza mikono yake katika mwili wa mwenzake.Rehema alianza kurudi nyuma polepole na kujikuta wanaanguka juu ya kitanda bila kujali.
  Muda ulienda na ndipo Mbaraka alikumbuka kwamba wakati huo alitakiwa awasili darasani.Ghafla alibanduka katika mikono ya Rehema na kumwambia “Samahani ratiba inanibana muda huu si unamjua Yule mwalimu Kesi anaweza kutoa kazi ya kushtukiza?”.Rehema hakufurahia kuambiwa vile kwani tayari alishajiachia kwa kila ambacho kingetokea,ila kwa vile alikuwa anampenda sana nakujali mafakio yake hakuwa na jinsi kumkubalia.Waliagana kwa mabusu motomoto na kila mmoja kuwa na furaha na mwenzake.
Mapenzi yao yalipamba moto na kujikuta wanaamua taarifa za uhusiano wao kuzipeleka kwa wazazi wa Rehema kwaajili ya ndoa. Baada ya wazazi wa Rehema kuwasili nyumbani walifurahia sana kupata taarifa hiyo ya mipango yao ya ndoa.Waliamini lilikua ni jambo la kheri na Mungu angewazidishia baraka katika maisha yao.
 Rehema hakuwa mnafiki kwa ahadi yake.Alimkabidhi Mbaraka zawadi ya nyumba yenye thamani ya mamilioni ya fedha iliyopo maeneo ya Mbezi.
 Miaka ilisogea na penzi lao lilizidi kukuwa, hata walifanikiwa kuhitimu shahada zao kutokana na bidiii zao.Mbaraka alifanikiwa kupata ajira katika kampuni moja maarufu ya uuzaji na usambazaji wa magari kutoka Japani akiwa kama msimamizi msaidizi wa kampuni hiyo maarufu iliyopo Posta jijini Dar es salaam.
SURA YA NANE
Ilikuwa jumapili majira ya saa tatu za asubuhi Mbaraka akiwa nyumbani kwake akijishughulishasha na uandaaji wa chai,ghafla zilianza kumjia fikra juu ya wazazi wake,kwani tangu aanze masomo yake ya chuo kikuu mpaka sasa ameshamaliza na kupata ajira hajawahi kwenda nyumbani zaidi ya salamu kwa njia ya simu  na kuwatumia fedha ili kukidhi mahitaji yao. Haikua desturi mbaya kuwatumia pesa ila ni vyema zaidi aende nyumbani siku akipata likizo kazini kuwaona wazazi wake waliofanikisha maendeleo na mafanikio yake.
Punde simu yake iliita.Hakuwa mwengine bali ni baba mkwe wake mtarajiwa mzee Said Lugomba.Aliipokea simu ile kwa heshima zote kwani alikuwa akimthamini na kumuheshimu sana.
Mzee nae alikuwa anampenda sana mkwe wake mtarajiwa.Alimtaka aweze kufika nyumbani siku inayofuata asubuhi kwaajili ya kikao cha maandalizi ya ndoa.Hakulipinga hilo zaidi ya kufurahi sana.Baada ya mawasiliano hayo alimpigia simu rehema na kumjuulisha taarifa hizo punde tu kutoka kwa baba yake.Naye Rehema alifurahi sana kusikia habari hiyo ambayo ilikua ndoto yake kwa muda mrefu.
Ama kweli daima ngoja ngoja inaumiza matumbo.Kwa kipindi chote hicho kijiji cha Wasahawa kilikosa furaha na amani.Kiliandamwa nahuzuni na vilio vya kuhuzunisha sana.Bahati hakuwa duniani wala akhera, hakuwa anaelewa liendalo wala lirudilo duniani.Kwa muda mrefu sasa yupo kitandani tu.
   “Sisi tunampenda sana ila Mungu atampenda zaidi”.Hayo ndio yalikuwa maneno ya waliowengi baada ya kuona kwamba Bahati hawezi kupona.Alinyooka kitandandani mithili ya nyoka aliemwagiwa mafuta ya taa kichwani pake.Alikuwa mwembamba aliyepoteza hata mvuto wa aina yoyote.Alikuwa hatamaniki tena hata chembe, utadhani hakuwa mrembo na mlimbwende wa aina yake,alikwisha kabisa,wazazi wake walishakata tamaa na kumsubiri Mungu amchukue siku aliyopanga.
   Kwa muda wote huo hawakujua ni nini haswa kinamsumbua Bahati,hakuwa anaonekana na maradhi aina yoyote kila alipotazamiwa.Kifo kilishaingia chumbani mwake,lakini moyo wake ulikuwa unafanya kazi moja tu yaupendo,kwani bado Mbaraka alikuwa moyoni mwake.Hakuna alietambua hilo zaidi ya mzee Mkata pekee,nae hakuweza kufichua siri hiyo ambayo alimuahidi kwamba atailinda na kuitunza daima.Ugonjwa wa mapenzi ulizidi kummaliza Bahati kila muda ulivyokuwa unasonga mbele.
  Mzee Mkata alianza kujawa na huruma juu ya maisha ya Bahati,alijuwa kwamba yeye alikua ndio mkombozi wa maisha yamwanawe,kwanini na yeye asikomboe uhai wake.Aliwaza na kuwazua bila kupata jawabu lolote,ila alitafakari kwa kina kwamba hata kama ataamua kumkomboa ataanzia wapi.Alishindwa afanye niniila hakukata tama.
 Siku ya jumatatu majira ya saa mbili asubuhi.Siku ambayo ilitayarishwa kwalengo la kumtakia maombi Bahati.Wazee na na vijana walikusanyika nje ya nyumba yao Bahati chini ya mti mrefu uliooteshwa kwa lengo la kuajiri upepo na kivuli kizuri. Hakikuwa kikao cha furaha kwani kila mmoja alionekana akiwa na huzuni zaidi ya mwenzake.
 Mzee Mkata na mke wake nao hawakuwa nyuma, walionekana wakikosa amani zaidi kwani wanampenda sana Bahati kwa tabia zake njema.Mkata alionekana kukosa amani kabisa huku akiurai na kuushawishi moyo wake juu ya hali ya ile. Baada ya dakika chache alisimama mzee mmoja aliyekuwa na kitambaa mkononi mwake.Hakuwa mwengine bali ni baba wa mgonjwa huyo mahututi.Kitambaa hicho hakikua kinatumika zaidi ya kufutia machozi.Aliwataka watu watulie na wae tayari kumsikiliza.
“Sawa mzee” watu waliitika kwa huzuni. 
Alianza kuwaambia “Bahati ndio yupo safarini kuelekea akhera, hivyo ninawaomba wanakijiji nyote ambao mmumehudhuria hapa tutumie nafasi hii kumtakia dua kwani hata mimi nimeshakata tama juu ya uhai wake”, alivuta pumzi kwa upole kisha akaendelea “tuamini kwamba Mungu ndie mpangaji wa kila jambo,yeye ndie anaemiliki pumzi zetu na kila kilichopo ulimwenguni,naamini sote tunaujua umuhimu wa kuwepo binti yetu ila huenda Mungu amepanga tofauti na matakwa yetu.Naomba tumuombee dua”. Mzee Hassan aliongea mengi zaidi ambayo yalizidi kuwapa watu masikitiko.Kila mmoja alijiinamia chini kuficha sura yake iliyotokwa na machozi.Baadhi ya kina mama walikosa nguvu na kujikuta wakilia kwa sauti kubwa huku wakipiga kelele kana kwamba tayari Bahati ameshaiaga dunia.
 Kijiji kilijiinamia kwa simanzi iliyotawala kwa kila mmoja.Jambo hilo lilimfanya mzee Hassan kushindwa kuongea mengi.Aliamua kukaa chini huku akijipangusa machozi kwa kutumia kitambaa chake ambacho ameshika mkononi mwake.Ghafla mama wa Mbaraka alihisi kizunguzungu na kujikuta akianguka katika bega la mume wake na kupoteza  fahamu.Tukio hilo lililozidi kumpa presha mzee huyo,alinyanyuka na kushika kichwa cha mke wake huku akimlaza chini polepole akiwa hana fahamu yoyote.Baada ya kuona tukio hilo mzee Hassan nae aliinuka mahala alipokuwa amekaa na kumtaka mzee Mkata ashirikiane na kina mama wengine kumuingiza ndani.Nao kwa haraka walifanya hivyo.Mzee Hassan alimuashiria mama Bahati asogee karibu yake na kumtaka aende ndani ili akaandae sehemu ya kuweza kumuhifadhi jirani yao kwa haraka.Aliingia ndani na kumtandikia eneo ambalo halikuwa mbali na Bahati kisha alitoka nje kumuashiria mume wake kwamba tayari ameshafanya hivyo na ndipo walishirikiana kumuingiza ndani.
  Kweli usilolijua ni sawa na usiku wa giza kwani baada ya mzee Mkata kuingia ndani aliangaza huku na huku katika purukushani hiyo.Bila kutarajia alimuona Bahati akiwa amelala kitandani. Moyo wake ulizidi kukatika kwa majeraha makubwa.Hakuweza kuvumilia tena maumivu ya kilasiku.Baada ya kumlaza mke wake alimuomba mzee Hassan ampe japo dakika chache za kwenda kumuona Bahati kitandani pale.Kwajinsi walivyokuwa marafiki hakuweza kumkatalia.
Mzee Mkata alisogea katika kitanda cha Bahati. Wakati alipokuwa akimtazama machozi yalimtoka nakuhisi kwamba yeye ndio sababu ya Bahati kuwa katika hali hiyo.Alianza kuyakumbuka yaleyote ambayo Bahati alimfanyia hadi kufanikisha ndoto za mwanawe.Kutokana na upeo wa akili na busara zake alizokuwa nazo mzee huyo aliweza kugundua kwamba mapenzi juu ya Mbaraka ndio yaliyomsukuma Bahati kufanya aliyoyafanya hapo awali.
Aliwaza mengi na kugundua kwamba maradhi ya Bahati yalianza punde tu pale Mbaraka alipoondoka kwenda kusoma.Maswali yalikuwa mengi kichwani mwake na baada ya kuunganisha matukio alipata jawabu kwamba maradhi ya Bahati ni kweli yamesababishwa na Mbaraka kwani alimpenda ila inwezekana alishindwa kumweleza na ndio mana yamemsibu maradhi yasio na tiba.
Maumivu makali yalitoboa moyo wake,  alijaribu kumuamsha Bahati ili aweze kumuuliza japo alihisi kuwa asingemtambua kutokana na kuugua maradhi hayo yaliyomkumba kwa muda mrefu.Alimuita kwa sauti ya chini “Bahati...Bahati mwanangu ni mimi mzee Mkata nipo hapa…”. Kilichomshangaza ni kumuona Bahati akilazimisha kufumbua macho yake na kuinua kichwa chake akimtazama aliekuwa akiongea maneno hayo.Kwa bahati mzuri aliweza kuitambua sura ya mzee huyo aliezoeana nae sana kipindi cha uzima wake.Alimzoea kwa nidhamu yake ya kupita na kumsalimia kila siku aendapo shambani kuwasaidia wazazi wake.
 Mzee mkata alizidi kumtazama Bahati kwa huzuni sana, wakati huo akiwa amesahau hali iliyomkuta mke wake na kwamba alihitaji uwepo wake ili apone. Ghafla Bahati alitamka kwa sauti ya chini kumuuliza mzee Mkata “umekuja na Mbaraka?”.
Mapigo ya moyo ya mzee huyo yalipiga kwa kasi mithili ya ngoma iliyogongwa kwa nguvu na kutoa mlio mkubwa uliosikika mbali.Aliamini kuwa alichokiwaza kilikuwa ni cha kweli na hakuwa na sababu ya kusubiri na kuendelea kumuacha Bahati akizidi kuteseka na kuichungulia akhera.Aliwaza vya kumjibu kwani alijua Mbaraka yupo mbali na haijuilikani siku ambayo atakuja  kijijini hapo.Aliamua kumdanganya ili kuupoza moyo wake “Mbaraka yupo njiani anakuja kijijini kwajili yako,sawa mwanangu!!”,Bahati alitabasamu.Kweli maradhi ya Bahati yalisababishwa na Mbaraka.
Mzee mkata aliwaza kufanya mawasiliano na Mbaraka ili aweze kuja kijijini haraka iwezekanavyo kuokoa maisha ya mtu aliyetimiza ndoto zake na mwenye upendo wadhati kwake.
Alitoka nje ya nyumba na kukuta wanankijiji wakiendelea kuulilia uhai wa Bahati.Kwa busara alimuita mzee Hassan na kumtaka awaamuru wanankijiji kurejea majumbani kwao.Ndipo wanakijiji walianza kutawanyika wakiwa wameshakata tamaa kuhusu maisha ya mpendwa wao.
Wazee hao waliitana pembeni kidogo ya nyumba na kuanza kuning’ona kwa sauti ya chini sana,bila shaka kulikuwa na siri kubwa iliyokuwa ikijadiliwa na wawili hao.Kwa mbali alionekana mzee Hassan akionesha sura ya mshangao wa  jambo ambalo hakuwa mwenye kuliamini.Waliamua kusogea pembeni zaidi na kukaa juu ya mkeka mkukuu ambao hata rangi yake haikuweza kuonekana vizuri kwa jinsi ulivyokuwa umechakaa.Mzee Mkata alimueleza mzee Hassan kwamba yeye anaelewa maradhi ya Bahati na alimtambua kwa muda mchache ambao alimruhusu kuongea nae.Mzee Hassan alishangaa na kudhania kwamba Mkata anaanza kuzeeka vibaya na labda akili zimeanza kumruka baada ya mke wake kupoteza fahamu.Alimuuliza “unamaanisha nini mzee mwenzangu?,au meanza kula chumvi nyingi sasa”.Mzee Mkata hakutaka kuongea mengi,alimtaka amsaidie mawasiliano ili awasiliane na mwanawe Mbaraka kwa ajili ya kuja kijijini.
Kama ilivyo kawaida ya Mzee Hassan, alikuwa anawajali sana wanakijiji kwa shida alizoweza kuwasaidia,ghafla alinyanyuka na kuingia ndani,hakuchukua muda mrefu alitoka akiwa ameshika simu ndogo mkononi mwake,alimkabidhi mzee Mkata na kumtaka afanye anayotaka kufanya.
 Wakati huo Mbaraka alishafika kwa kina Rehema akisubiri kikao kianze kama alivyoahidiana na mzee Saidi.Kikao ambacho alikwishaelewa dhamira yake ilikuwa ni matayarisho ya ndoa yake na mpenzi wake Rehema.Wakiwa ukumbini yeye na mama mkwe wake pamoja na mke wake mtarajiwa wakimsubbiri mzee Saidi afike ghafla simu yake iliita.Hakuwa mwengine ila ni baba yake kwani alikuwa na kawaida ya kutumia simu ya Mzee Hassan pindi anapotaka kuwasiliana nae. Kwa haraka na heshima aliipokea simu hiyo.Ila punde tu baada ya sekunde chache uso wa Mbaraka ulionekana kuanza kupata huzuni kila alipokuwa anazidi kuongea.Rehema alishtuka kumuona mpenzi wake amebadilika ghafla, alianza kuelewa kwamba haikuwa simu ya furaha.
 Mbaraka alikata simu na kubaki kama bumbuwazi.Rehema aliwajibika kumtuliza na kutaka kujua nini kinaendelea.Nae mama mkwe wake mtarajiwa hakuwa mbali na hilo alimshawishi Mbaraka aongee nini tatizo.Mbaraka hakuona sababu ya kukaa kimya na kuzidi kupoteza muda bali aliwataka samahani na kuwaambia kwamba alietoka kumpigia simu ni baba yake mzazi na anamtaka aende nyumbani haraka iwezekanavyo.
 Rehema alishtuka kusikia hivyo kwani alitambua kwamba kutokana na ghafla hiyo hakutokuwa na salama.Mbaraka hakutaka kukaa sana hapo ila aliamua kuenuka juu ya kochi,aliwaaga na kuwaambia wamvumilie na wamsamehe kwa hili lililotokezea mpaka atakaporudi ndani ya siku mbili.
 Kwa vile baba mkwe wake alikuwa hajafika hapo aliwataka wampe salamu kwani Mbaraka alimuheshimu sana baba yake na hakuweza kupinga chochote kutoka kwake katika hali yoyote ile.
Kutokana kwamba hakujua nini kilichotokea huko aliamua kutekeleza na kuitikia wito huo ipasavyo.
“Sawa mwanangu safari nakutakia safari njema njema”.Maneno hayo yalisemwa na mamamkwe wake mtarajiwa.
Wakati anaondoka Rehema alimfata nyuma huku akiwa na huzuni juu ya wito wa Mbaraka kijijini.Alimtaka waende wote lakini mbaraka hakupenda Rehema ajumuike katika safari hiyo kwasababu hakujua anaitiwa jambo gani na alitegemea kurudi mapema tu kwasababu yuko kazini.
 Kwa vile Rehema alikuwa anatembea katika kivuli cha Mbaraka ambae ni mume wake mtarajiwa hakuacha kuwa king’ang’anizi juu ya hilo,hatimaye aliyaelewa maneno ya hekima ya mpenzi wake ambae alikuwa ndoto yake kwa muda mrefu.Mbaraka alineua mikono yake na kumruhusu Rehema aweke yakwake juu ya viganja vyake.Alishika mikono ya Mbaraka na kukumbatiana huku mioyo yao ikiuma kwa kutaka kutengana kwa muda wa siku chache.Rehema alizidi kutokwa na machozi mengi zaidi kwani hakujua ni nini ambacho kimejiri huko kijijini. Lilikuwa ni fumbo lililoushinda moyo wake kulifumbua.
“sawa safari njema mume wangu,elewa nakusubiri wewe tu kwa ajili yakufunga ndoa.” mdomo wake ulijikaza kutamka hilo na kuiusia nafsi yake subra na uvumilivu juu ya kiza cha siku chache.
“usijali mke wangu,nitarudi kwa ajili yako baada ya siku mbili,siwezi kukuacha ukateseka kwa ajili yangu,na hata mimi sitoweza kuutesa moyo wangu kwa kukaa mabli na wewe.Nakupenda sana mke wangu,nisubirie”.Baada ya kuogea hayo Mbaraka alitoka ndani ya nyumba hiyo ya kifahari na kuanza kutembea kwa mwendo wa unyonge kuelekea barabara kuu kufikia kituo cha daladala.Wakati anatembea kichwa chake kiliyageuza macho yake nyuma yakiwa yanamtazama Rehema aliekuwa nje ya geti akimsindikiza kwa macho ya unyonge.
  Mbaraka alifika kituoni na kupanda daladala iliyokuwa inaelekea Mbezi.Alifika nyumbani kwake majira ya saa sita za mchana.Aliingia chumbani kwake ili kujiandaa kwa safari hiyo ya ghafla.
Baada ya muda alitoka nje akiwa amevaa vizuri na begi dogo alilokuwa amelibeba mgongoni kwake.Alitoa simu yake na kutuma ujumbe mfupi wa maandishi kwa bosi wake wa kampuni ambayo anafanyia kazi ili kutaka kumjuilisha kuhusu safari hiyo ya ghafla kwani alijua kwa wakati huo simu ya bosi wake haitakuwa hewani kutokana na pirika za kikazi,hivyo asingeweza kuwasiliana nae.
Alisogea kwenye kituo cha bodaboda,madereva wa bodaboda kama kawaida yao walichangamkia kazi  kama inzi wakati wakutapo chakula chao wakipendacho.Mbaraka alichukuwa bodaboda kuelekea stendi ya mabasi Ubungo.
Aliwasili stendi ya mkoa mnamo saa saba za mchana.Sauti za madalali wa mabasi ya abiria ziliskika kwa wingi,kila mmoja alianza kumsogelea na kumpa sifa za gari lake ili ashawishike nalo.Kelele zilikuwa nyingi ambazo ziliweza kusababisha hata wengine kuanza kukingiana vifua kutokana na tamaa na njaa ya nchi yao.Mbaraka alitoa simu yake na kuangalia muda.Kwakweli dakika na sekunde zilikuwa zinatembea kwa kasi huku sauti za “Mbeya!!, Mbeya!!!, Iringa mapema, Moshi !!!, Moshi!!!” zikisikika kwa fujo.Alisubiri asikiye sauti inayonadi Morogoro,nayo haikuwa mbali kwani ilisikika ghafla “haya Morogoro!!Morogoro!!mapema”, aliifuata sauti hiyo na kuanza kuchangamkiwa kama msanii maarufu kutoka ulaya.

Aliingia ndani ya basi hilo huku mawazo mengi yakiwa yamemtawala kichwani mwake.Hakujuwa ni nini haswa kimejiri nyumbani kwao.Wakati huo mawazo ya Rehema yalimjia ghafla kutokana na mazoea na ucheshi wa mapenzi yao.

ANAEHITAJI KITABU HICHI TAFADHALI WASILIANA NAMI KUPITIA 0658745759.
BEI NI NAFUU SANA ELFU 5 TU.